• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
      • Maji
      • Huduma ya Menejimenti ya Serikali za mitaa
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Menejimenti ya Serikali za mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

TANROADS Yaamua Kuendelea na Ujenzi wa Barabara ya Kikusya-Ipinda-Matema

Imetumwa : March 15th, 2018

SERIKALI kupitia Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Mbeya, imeamua kuendelea na ujenzi wa barabara ya Kikusya – Ipinda – Matema katika Wilaya ya Kyela, licha ya baadhi ya wakazi wa Mji wa Ipinda kufungua kesi mahakamani kupinga nyumba zao kubomolewa.

Akitoa taarifa ya ujenzi wa barabara hiyo kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla, msimamizi wa mradi huo kutoka katika Kitengo cha ushauri wa kihandisi TANROADS (TECU), Mhandisi Samwel Mwambungu, alisema kitendo cha wananchi hao kufungua kesi kimesababisha mradi kuchelewa kukamilika.

Mhandisi Mwambungu amesema kutokana na umuhimu wa barabara hiyo kwa wananchi wa maeneo hayo, wameamua kuendelea na ujenzi kutokana na eneo lililopo huku nyumba za wananchi hao zikiachwa kama zilivyo.

Mhandisi Mwambungu, amesema barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 34.6 inajengwa kwa kiwango cha lami na Mkandarasi China New Era International Engineering Corporation kwa gharama ya shilingi milioni 56.9 na kwamba mradi unatekelezwa na serikali kwa asilimia 100.

“Mradi ulianza kutekelezwa julai 31, 2015 na ulitakiwa kukamilika ndani ya miezi 24, lakini mpaka sasa haujakamilika kutokana na baadhi ya changamoto ikiwemo baadhi ya wananchi kufungua kesi mahakamani wakipinga kupisha upanuzi,” alisema Mhandisi Mwambungu.

“Tumeamua tuendelee na ujenzi lakini kwenye eneo ambalo hawa wananchi wamegoma, tunajenga kulingana na eneo lililopo bila kugusa nyumba zao,”

Vilevile alisema Mkandarasi wakati mwingine huwa anakwama kutokana na Serikali kumcheleweshea malipo yake, kwa maelezo kuwa mpaka sasa amelipwa shilingi bilioni 7.2 kati ya bilioni 26 anazodai kulingana na kazi aliyoifanya.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Amos Makalla, ameshangazwa na kitendo cha wananchi hao kuishtaki Serikali kwa madai kuwa barabara hiyo ni faida yao wenyewe na hivyo walichokifanya wanajiumiza wenyewe.

Mhe. Makalla amesema barabara hiyo ikikamilika itafungua fursa nyingi kwao ikiwemo kurahisisha usafiri na usafirishaji wa mizigo kutoka katika maeneo yao na kupeleka maeneo ya masoko ikiwemo kupeleka Kyela mjini na Mbeya.

Aidha Mhe Makalla amesema barabara hiyo itafungua fursa kwenye sekta ya utalii kwa madai kuwa fukwe za Ziwa Nyasa katika eneo la Matema ni kivutio kikubwa cha watalii hivyo wananchi hao watanufaika kwa kuwaongoza watalii na kuwauzia bidhaa mbalimbali wanazozalisha.

“Mtunze kumbukumbu vizuri kwa kile mlichokifanya hapa, watoto wenu na wajukuu watakapowauliza kwanini barabara nyembamba hapa, mkawambie tuliipeleka serikali mahakamani ndio maana ikaamua kujenga hivyo,” alisema Makalla.

Hata hivyo Makalla amesema anakusudia kwenda kuonana na Waziri wa Ujenzi Prof. Makame Mbarawa ili kushawishi Mkandarasi wa barabara hiyo aendelee kulipwa fedha za mradi huo pamoja na kumuomba aidhinishe kipande kinachobakia kuanzia Tenende kwenda Kyela kiunganishwe kwenye Mkataba.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Claudia Kitta, aliishukuru Serikali kwa kuamua kujenga barabara hiyo akidai kuwa itakuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo.

Alisema ni nadra barabara ya kiwango kama inayojengwa katika eneo hilo kutoka mjini kwenda kijijini, hivyo akawataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Mkandarasi.

Matangazo

  • Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza 2021 Mkoa wa Mbeya. December 18, 2020
  • Matokeo ya Kidato cha Sita 2020 August 21, 2020
  • Matokeo ya Darasa la Saba 2020 November 21, 2020
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • Mkoa wa Mbeya Wajiwekea Malengo ya Upandaji miti

    January 13, 2021
  • Mbeya Yaja na Mkakati Mpya wa kupunguza Upungufu wa Vyumba Vya Madarasa

    December 09, 2020
  • Mbeya Waadhimisha Siku ya Uhuru kwa Kupanda Miti

    December 09, 2020
  • RC Aagiza Kuchunguza Upotevu wa 800M za Walimu

    December 04, 2020
  • Tazama Zaidi

Video

Viongozi watakiwa kuwa wasafi
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Wasifu wa Mkoa wa Mbeya 2015
  • Mpango Mkakati wa Mkoa 2018-2023
  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Mpango Mkakati wa Kuendeleza Sekta za Kilimo 2020 - 2025
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Tovuti ya Serikali
  • TAMISEMI
  • Ajira

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Uzunguni Road

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025 2503034

    Simu ya Mkononi: 255 784838650

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright ©2019 Mbeya Region . All rights reserved.