• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Chagueni Viongozi Wachapakazi- Mama Samia

Imetumwa : July 28th, 2018

MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu, awataka viongozi wa Mkoa wa Mbeya kuendana na kasi Serikali ya awamu ya tano ili kufikia malengo yake ya kufikia uchumi wa kati na kwamba viongozi ndio wenye uwezo wa kuwaonyesha wananchi njia sahihi ya maendeleo.

Samia aliyasema hayo juzi jijini Mbeya, baada ya kupokea taarifa ya mkoa huo iliyowasilishwa na Mkuu wa mkoa, Amos Makalla, ambapo alisema ili wananchi wapate maendeleo ni lazima wapate viongozi bora na wachapakazi

 Mama Samia amewataka wananchi wa Mbeya kutumia Uchaguzi wa viongozi wa Serikali za Mitaa mwakani kuchagua viongozi wenye fikra za maendeleo na wachapakazi ili kuendana na kasi ya Serikali iliyopo madarakani.

 “Nitumie nafasi hii kuwashauri wananchi wa mkoa wa mbeya, katika uchaguzi wa viongozi wetu wa serikali za mitaa, mkatuchagulie viongozi wachapakazi na wenye maono ambao mna uhakika wataendana na kasi ya serikali yetu inayotaka maendeleo,” alisema Samia.

Akisoma Taarifa ya Mkoa wa Mbeya Mkuu wa Mkoa Mh Makalla alisema wananchi wa mkoa huo kwa sasa hawafanyi siasa kama ilivyokuwa miaka ya nyuma na badala yake wanafanya kazi kwa nguvu ili kujiletea maendeleo.

Makalla alisema kuwa wananchi hao wamekuwa wakishiriki shughuli mbalimbali za maendeleo kwa ushirikiano bila kujali tofauti za itikadi za kisiasa hali iliyoufanya mkoa huo kufanya vizuri kwenye miradi mbalimbali inayopelekwa na serikali.

Alisema mkoa huo kwa sasa umeshika nafasi ya nne katika uchangiaji wa pato la taifa ukitanguliwa na mikoa ya Dar es salaam, Mwanza na Shinyanga na kwamba unachangia asilimia 5.3.

“Wananchi kwa sasa wameweka pembeni siasa wanachapa kazi, wananchi hawa hawasukumwi kufanya kazi, ukiwashirikisha suala lolote la maendeleo wanaitikia vizuri ndio maana sisi ukiambiwa kituo cha afya kinajengwa, wananchi wanajitokeza kuchangia,” alisema Makalla.

Aidha alisema changamoto kubwa inayoukabili mkoa huo ni takwimu za maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU), kuwa juu kuliko kile kiwango cha kitaifa.

Alisema maambukizi ya Ukimwi katika mkoa huo ni asilimia 9.3 huku kitaifa ikiwa asilimia 4.7 na kwamba mkoa huo ni wa tatu baada ya Njombe na Iringa hivyo akasisitiza kuwa hiyo sio sifa nzuri.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), mkoa wa Mbeya, Jacob Mwakasole, alisema chama hicho kinaridhishwa na utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya mwaka 2015 unaofanywa na viongozi wa serikali.

Alisema utekelezaji huo unawafanya wananchi mkoani humo kuanza kukiamini chama hicho kuliko ilivyokuwa awali ambapo wengi walikuwa wanaonekana kuwa ni wapinzani.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa