• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Halmashauri ya Jiji Yapewa Siku 3

Imetumwa : March 11th, 2021

MKUU wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila ametoa muda wa wiki tatu kwa uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya kuandaa mpango kazi utakaoainisha mahitaji mbalimbali ya watoto wenye mahitaji maalum katika Shule ya Msingi Itiji na kasha kupeleka wa wadau na Serikali ili kusaidia.

Chalamila alitoa maagizo hayo juzi wakati alipofantya ziara ya kutembelea shule hiyo na kuangalia mazingira wanayosoma watoto wenye mahitaji maalumu.

Kulingana na mazingira aliyoyakuta ambayo hakuna vyoo kwa ajili ya watoto wenye mahitaji maalum, vifaa vya kujifunzia na eneo la michezo alimwagiza Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, William Ntinika kwa kushirikiana na viongozi wenzake kuandaa andiko ambalo litaainisha mahitaji yote ya muhimu kwa ajili ya kuwasaidia watoto wenye mahitaji maalum ili wasome kwa furaha.

“Nawapongeza walimu kwa kazi nzuri mnayoifanya licha ya kufundisha kwenye mazingira magumu lakini mnapambana, nimeona hakuna vyoo rafiki kwa watoto wenye mahitaji maalum hapo wanatumia vya watoto wa kawaida lazima tuwashirikishe wadau kusaidia ujenzi huo” alisema Chalamila.

Alisema shule ya Msingi Itiji ni miongoni mwa shule jumuishi ambao zinakabiliwa na vikwazo mbalimbali ikiwemo miundombinu ya madarasa, vyoo, vitendea kazi na maeneo ya michezo.

Aidha alishauri uongozi wa shule hiyo kufanya mawasiliano na walimu wa Shule ya Msingi Makalala iliyopo mjini Mufindi mkoani Iringa kujifunza namna walivyofanikiwa kuendesha shule hiyo yenye watoto wenye mahitaji maalum na kawaida.

Aliwaagiza viongozi wa Jiji kutenga bajeti kwa ajili ya ujenzi wa bweni ili kuwasaidia watoto wenye ulemavu ambao wanatoka mbali kukaa shuleni na kupunguza tatizo la utoro pamoja na madhara mengine ambayo yanaweza kutokea wakati wa kwenda na kutosha shuleni.

Kutokana na mazingira hayo, Chalamila alitoa msaada wa fedha kiasi cha shilingi milioni moja kwa ajili ya kuanza ujenzi wa vyoo huku akiwaagiza viongozi wengine kuchangia ili kukamilisha ujenzi wa matundu sita ya vyoo pamoja na ujenzi wa hosteli kwa ajili ya watoto hao.

Akizungumzia tatizo ya uhaba wa matundu ya vyoo kwa ajili ya watoto wenye mahitaji maalum, Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Jerome Kayange alisema jumla ya watoto 92 wanasoma hapo na kwamba kati ya hao 574 ni watoto wa kawaida.

Alisema shule hiyo ni jumuishi na kwamba miundombinu iliyopo ni rafiki kwa watoto wa kawaida, aliiomba Serikali na wadau wengine kuendelea kuwasaidia ili watoto kusoma katika hali ya utulivu.

Alisema shule hiyo ina jumla ya walimu 20 na kwamba kati yao wanawake ni 17 na wanaume watatu kati yao walimu tisa wakifundisha watoto wenye mahitaji maalum.

Mwalimu anayefundisha watoto wenye matatizo ya akili, Clement Nyabumbwe alisema vifaa vya kujifunzia havikidhi mahitaji kwa madai kuwa watoto wenye shida hiyo muda mwingi wanahitaji shughuli za kufanya na michezo mbalimbali.


Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa