• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Halmashauri za Vijiji Zatakiwa Kuwa na Mpango Bora wa Ardhi

Imetumwa : March 8th, 2020

Hayo yamesemwa na mjumbe  wa Kamati Maalumu ya Uelimishaji Wananchi Juu ya Umuhimu wa Uhifadhi na Ujirani Mwema, Afisa Mipango Miji Kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Ndg. Enock Kyando alipokuwa akiwasilisha mada yake ya matumizi bora ya Ardhi katika vijiji vya Uturo, Mtamba, Ukwama na Kapunga Wilaya ya Mbarali siku ya tarehe 07/03/2020.

Kyando alisema kuwa wanakijiji wanapaswa kuzisimamia Serikali zao za kijiji ili ardhi yao isichukuliwe bila kufuata utaratibu kwani kuna baadhi ya sehemu baadhi ya viongozi wamekuwa sio waaminifu wanagawa ardhi ya kijiji bila kuwashirikisha wenye ardhi yao.

*“Msimamizi mkuu wa ardhi ya Kijiji ni Serikali ya kijiji kupitia mkutano mkuu, mtu yeyote anaehitaji kumiliki ardhi ya kijiji anatakiwa kupitishwa kwenye mkutano mkuu ili apangiwe matumizi ya ardhi aliyoiomba, Mtendaji na Mwenyekiti kazi yao ni kupokea maombi tu, Ardhi ni kitu cha muhimu, tusipoisimamia vizuri tutakuja kupigana wenyewe kwa wenyewe”* alisema Kyando

Kyando aliongeza kuwa kijiji kinatakiwa kuwa na mpango wa matumizi bora ya ardhi kwani itaondoa migogoro ya mipaka mbalimbali vilevile ni chombo kinachoonesha ni kiasi gani cha ardhi kilichopo kwa ajili ya shughuli za kijiji kama mifugo, kilimo, makazi, viwanda pamoja na matumizi mengine.

Aliongeza kuwa sambamba na kuwa na matumizi bora ya ardhi ya kijiji ni vizuri kila mtu mwenye kipande cha ardhi akachukua hati yake ya kimila yake  ambayo inapatikana ofisi ya kijiji ili awe amemiliki kisheria kwani Hati  miliki ya kimila ina hadhi sawa na hati miliki zingine za ardhi.

Aidha, Mjumbe mwingine wa timu ya uelimishaji Afisa Mipango Miji Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Ndg Geofrey Mwaijobele amesema kuwa ardhi haiongezeki bali wanadamu na mifugo ndio vinaongezeka kwa kasi hivyo ni muhimu Serikali za vijiji kuweka kipaumbele mpango wa matumizi bora ya ardhi ili kuepusha migogoro ya wakulima na wafugaji.

Mwaijobele ameongeza kuwa kama maeneo ya misitu na malisho ya mifugo yamehifadhiwa na kijiji ni vyema kila mwananchi akahusika kuyalinda maeneo hayo.


Baadhi ya wananchi waliohudhuria kwenye mikutano hiyo wameishukuru timu ya uelimishaji iliyoundwa kwani wameongeza uelewa wa masuala ya uhifadhi, kwani walikuwa wanavunja sheria bila kujiua na kupitia elimu hiyo watawaelimisha na wengine ili kudumisha ujirani mwema na wahifadhi.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • RC DKT. HOMERA AKUTANA NA MABALOZI WA NCHI NNE AFRIKA

    May 26, 2025
  • "WAFUNDISHENI PIA ULAJI WA LISHE WATU MAOFISINI" - RC DKT. HOMERA

    May 26, 2025
  • FISTULA INATIBIKA, MATIBABU NI BURE, KARIBU UHUDUMIWE - DKT. HOMERA

    May 19, 2025
  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa