• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Halmashauri zatakiwa Kutenga Fedha za Afua za VVU na UKIMWI

Imetumwa : December 1st, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe Albert Chalamila ameziagiza halmashauri zote za Mkoa wa Mbeya kutenga fedha kutoka vyanzo vya ndani ili kuendelea kutekeleza afua VVU na UKIMWI hasa kwa kinga na tiba ili kufikia malengo ya Mkoa ya kupunguza maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI.

Mhe Chalamila ametoa maagizo hayo leo Disemba 1, 2020 kwenye maadhimisho ya kilele cha Siku ya UKIMWI duniani yaliyofanyika viwanja vya Barafu Kata ya Rujewa Wilaya ya Mbarali na kusema kuwa kunahitajika rasilimali za kutosha hasa kipindi kwa kuwa rasilimali kutoka kwa wadau zimepungua kwa kiasi kikubwa.

Amesema kuwa Ili kuongeza kasi ya kuzuia maambukizi mapya ya VV na hatimaye kutokomeza kabisa maambukizi hayo, Mkoa kwa kushirikiana na wadau wengine, umeamua kutekeleza mikakati ya kuzuia maambukizi mapya ya VVU kwa njia mbalimbali kama: kutoa elimu ya mabadiliko ya tabia, ushauri nasaha na upimaji wa VVU ,  upimaji binafsi wa VVU, tohara kwa wanaume nk.

Mhe Chalamila amesema kuwa kutokana na takwimu za utafiti wa viashiria vya UKIMWI ya mwaka 2016/17 inaonyesha maambukizi ya VVU ni makubwa kwa kundi la vijana na hasa  mabinti wa umri wa kati  ya miaka 15-24.

“Kwa kweli tukikaa kimya hali Mbeya ukiangalia hata matukio ya kubaka yameshamili sana jambo ambalo ni kichochoe kwa hali ya kupanda kwa maambukizi na kufikia asilimia 9.3 kimkoa na kufika nafasi ya tatu kitaifa

Akisoma taarifa ya Mkoa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Dkt Salum Manyata amesema   kuwa Mkoa wa Mbeya umeshika nafasi ya tatu kitaifa kwa kuwa na asilimia 9.3 ya maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi huku waathirika wakubwa ni wasichana wenye wa chini ya miaka 24 kwa asilimia 70.

Dkt Manyata amesema  kuwa sababu kubwa ya kundi kuathika kwa kiwango hicho ni kutokaa na mihemko ya kushiriki tendo la ndoa wakiwa na umri mdogo hususan kwa watu waliowazidi umri.
"Licha ya wasichana pia asilimia 30 ya vijana ni wahanga hivyo kuna kila sababu ya kuwa na mpango mkakati wa pamoja ili kunusuru kundi hilo kwani ni nguvu kazi kwa taifa katika kuelekea uchumi wa viwanda "alisema

Aidha amesema kuwa takwimu zinaonyesha vijana walio katika kundi hilo 200 kwa siku wanambukizwa ukimwi huku kwa mwezi ni 6,000 hivyo ni jukumu la wadau mlioshiriki maadhimisho hayo kutafuta mwarobaini wa pamoja ili kuiweka Tanzania ikiwa Salama.

Mratibu wa tume ya kudhibiti UKIMWI(TACAIDS) Mkoa Emmanuel Petro, alisema kwa kipindi cha Oktoba 2019 mpaka Septemba mwaka huu jumla ya wakazi 217,762 walipima afya ambapo 11,185 walipatikana na maambukizi mapya ya Virusi vya ukimwi.Aidha alisema kwa kipindi hicho wajawazito 81,525 walipimwa ambapo kati ya hao 2,063 walikutwa na maambukizi na kuanza kupatiwa tiba na afya zao zinaendelea vizuri.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa