• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Hati Yenye Mashaka Chunya, RC Atoa neno

Imetumwa : June 9th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe Juma Homera amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Chunya kuwasimamisha kazi na kuwachukulia hatua Watendaji wa Kata 7 kwa tuhuma za kusababisha upotevu wa zaidi ya sh. Milioni 400 ambazo ni mapato ya ndani ya halmashauri mpaka watakaporudisha fedha hizo.

Mhe Homera ameongea hayo leo tarehe 09 Juni, kwenye kikao cha watumishi wa halmashauri hiyo na kusikitishwa na hali duni ya ukusanyaji wa mapato na upotevu wa mapato hayo kutoka kwa watendaji wa halmashauri

“ Sasa nakuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri kuwasimamisha hawa watendaji wote waliosababisha halmashauri kupata hati yenye mashaka kwa wao kukaa na fedha bila kuzipeleka benki kama utaratibu na kanuni zinavyotaka” Mhe  Homera

Amesema kuwa watendaji wa kata kwa kushirikiana na watendaji wanatumia fedha mbichi za halmashauri ambazo hazikupelekwa benki baada ya kukusanywa kutoka maeneo mbalimbali kinyume na kanuni na taratibu za halmashauri hiyo.

Aidha, Akiongea kwenye kikao hicho Katibu Tawala wa Mkoa Dkt Angelina Lutambi amewataka wataalamu hao kufanya kazi kwa weledi wakizingatia taratibu na kanuni za serikali na pia kufanya kazi ya kukusanya mapato kwa kushirikiana kuanzi idara ambazo vina vyanzo vya mapato ili yakusanywe kikamilifu.

“Suala la ukusanyaji wa mapato ni la lazima kwa kuwa Serikali ina majukumu makubwa ya kuwahudumia watumishi, kuhakikisha huduma zote zinatolewa na wananchi wananufaika na pia kuendesha serikali kwa hiyo ni wajibu wetu kuhakikisha tunakusanya mapato kikamilifu” Dkt Lutambi

Dkt Lutambi ameagiza kila Mkuu wa Idara kuhakikisha anapitia vyanzo vyote vilivyopo kwenye Idara yake na kuhakikisha anavisimamia na kukusanya mapato kwa kushirikiana na maafisa mapato wa halmashauri.

Naye Mbunge wa Jimbo la Lupa Masache Kasaka amesema kuwa halmashauri lazima iangalie imekosea wapi kuweza kujua wapi imejikwaa na pia amewataka watumishi wa halmashauri kutimiza wajibu wao kwenye kila Idara katika kusimamia ukusanyaji wa mapato ilituweze kutoka hapa tulipo.\

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa