• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Homa ya Mapafu Chanzo cha Kifo cha Dereva

Imetumwa : February 1st, 2021

Kamati ya watu saba iliyoundwa naMkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe Albert Chalamila kuchunguza kifo cha dereva wa lori, Abrahaman Issa imebaini kuwa ugonjwa wa homa ya mapafu ndio chanzo cha kifo cha mkazi huyo wa Temeke jijini Dar es Salaam.

Mhe Chalamila ametoa taarifa ya kamati hiyo leo Jumanne Februari2, 2021 katika mkutano wake na waandishi wa habari aliyoiunda kusaka ukweli wa kifo cha dereva huyo kilichozua utata baada ya wenzake kudai alifia kituo cha polisi huku polisi wakieleza kuwa alikufa baada ya kufikishwa hospitali na kwamba alikuwa na homa ya mapafu.

“Kamati iliyohusisha vyombo vya dola imefanya uchunguzi wa kina uliohusisha madaktari bingwa walichukua sampuli za vipimo katika kichwa na kifua ili kujiridhisha kama kunaweza kukawa na shida ambayo aidha ilitokana na kipigo au.”

“Lakini ilibainika tatizo ni homa kali ya mapafu na kabla ya kupatwa na tatizo hilo alikuwa na tatizo la pumu kwa kipindi kirefu. Unajua pumu au homa ya mapafu haistahili mtu kukaa kwenye chumba chenye baridi, licha ya afya yake kudhoofu huenda ilichangia kudhoofika zaidi na kusababisha umauti kumkuta kutokana na kukaa kituo cha polisi kwa masaa kadhaa,” amesema Chalamila.

Kuhusu sehemu aliyofariki dunia, Chalamila amesema,” kamati ilibaini afariki dunia saa 3 usiku akiwa katika gari la polisi akipelekwa kupatiwa matibabu katika kituo cha afya igawilo jijini Mbeya.”

Amesema Issa alipofikishwa katika kituo hicho daktari aliyekuwa zamu alibaini kuwa alikuwa amefariki dunia, mwili wake ulihifadhiwa.

Chalamila amesema amemuagiza kamanda wa polisi Mkoa wa Mbeya, Ulrich Matei kugharamia shughuli zote za mazishi ya Issa.

"Nimezungumza na ndugu wa marehemu kama watakuwa tayari kuchukua mwili kwa mazishi nimetoa kibali leo na kama hawajaridhishwa na majibu ya kamati kama Serikali tutawasikiliza uamuzi wao,” amesema.

Awali mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi wa malori, Abubakar Msangi amesema baada ya kupatiwa ripoti hiyo ndio watatoa majibu.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa