• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mama Lishe na Wapiga Debe Stendi Kuu Mbeya Kusajiliwa na Kutambuliwa kwa Shughuli Zao

Imetumwa : May 7th, 2018

Serikali Mkoa wa Mbeya imeiagiza Halmashauri ya Jiji kuweka utaratibu mzuri wa kuwatambua na kuwasajili wapiga debe na mama lishe wanaofanya shughuli zao eneo la stendi kuu ya mabasi kama wafanyakazi wa eneo hilo ili kuwajengea mazingira mazuri ya kufanya kazi zao.

Hayo yamesemwa leo na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Amos Makalla alipokuwa akikabidhiwa jengo la abiria lililofanyiwa ukarabati na halmashauri hiyo kwa kushirikiana na kiwanda cha soda cha Pepsi.

Mhe. Makalla amesema kuwa ni vizuri kuwatambua vijana hao rasmi kwa shughuli wanazozifanya za kujiingizia kipato ili kuondokana na adha wanayoipata ya kukamatwa na askari wa Jeshi la Polisi kila mara wanapokuwa kwenye shughuli zao.

“Halmashauri ya Jiji mnatakiwa mjipange kuwawezesha vijana hawa kuwa na vitambulisho na sare zao hata kwa kuomba kusaidiwa kutoka kwa makampuni mbalimbali yaliyopo hapa kuepusha vijana hawa kurudi mtaani na kuanza shughuli za uvunjifu wa sheria” amesema

Aidha, Mhe. Makalla ameipongeza halmashauri kwa kuweza kutoa fedha kutoka Serikalini na Kata ya Sisimba za ukarabati wa jengo la abiria kama alivyoagiza baada ya awali kulitembelea na kuona jinsi lilivyokuwa limeharibika.

Pia Mhe Makalla amemshukuru Mkurugenzi wa Kiwanda cha Pepsi tawi la Mbeya kwa kuweza kuchangia ukarabati huo kwa kuingiza mfumo wa umeme na kujenga viti kwenye jengo hilo kwa ajili ya abiria.

Awali akisoma taarifa ya ukarabati wa jengo hilo Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji Dkt. Amani Kilemile amesema kuwa ukarabati wa jengo hilo umefanywa na mkandarasi Bakanja Investment LTD na ulianza tarehe 31/08/2017 kwa gharama za shilingi 32,117,712/= kutoka ruzuku ya Serikali na shilingi 5,616,300 mchango kutoka Kata ya Sisimba.

Dkt Kilemile amesema kuwa halmashauri imelifanyia ukarabati jengo hilo kwa lengo la kuhakikisha kunakuwepo na usalama wa abiria na mali zao wawapo stendi na kuondokana na adha waliyokuwa wanaipata.

Akitoa changamoto za watumiaji wa stendi hiyo Diwani wa Kata ya Sisimba Mhe. Geofrey Kajigili amelalamikia kutokuwepo na choo bora kwa ajili ya abiria kwani choo kilichopo ni kibovu na hakifai kwa matumizi ya binadamu.

Aidha, Mhe Kajigili ameiomba Serikali kuangalia uwezekano wa kuhakikisha wanakarabati taa za stendi ambazo zina muda mrefu haziwakiwa na hivyo kuwapa wakati mgumu wafanyabiashara wadogo hasa mama ntilie wanaofanya kazi hadi usiku.

Mhe Kajigili ameiomba halmashauri pia kutoa elimu kwa wafanyabiashara walioambiwa wakarabati vibanda vyao kwa kuwa wamekuwa na wasiwasi wa kupandishiwa bei ya kodi baada ya zoezi hilo.

Ukarabati wa jengo la kusubiria abiria kituo kikuu cha mabasi ulianza tarehe 31/o8/2017 baada ya agizo la Mkuu wa Mkoa wa Mbeya kwa halmashauri alipotembelea na kuona ubovu wa jengo hilo.   

 

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • RC DKT. HOMERA AKUTANA NA MABALOZI WA NCHI NNE AFRIKA

    May 26, 2025
  • "WAFUNDISHENI PIA ULAJI WA LISHE WATU MAOFISINI" - RC DKT. HOMERA

    May 26, 2025
  • FISTULA INATIBIKA, MATIBABU NI BURE, KARIBU UHUDUMIWE - DKT. HOMERA

    May 19, 2025
  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa