• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mbeya Region Defense and Security Committee Visited Itungi Port

Imetumwa : April 11th, 2017

Kukamilika kwa utengenezaji wa Meli za Mizigo na abiria katika Bandari ya Itungi  kutafungua fursa za kiuchumi na kufungua fursa za kimapato kwa Wananchi na Serikali na kupunguza gharama za uendeshaji wa biashara kwa kutumia miundombinu ya barabara.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe Amos Makalla wakati Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa ilipofanya ukaguzi wa utengenezaji wa Meli tatu mpya za Mizigo na Abiria katika Bandari ya Itungi Wilayani Kyela.

Mhe. Makalla amesema kuwa kukamilika kwa Meli hizo kutasaidia usambazaji wa bidhaa mbalimbali ambazo viwanda vilivyopo Mbeya vinapata shida kuzunguka kupata. Aidha, mradi huu utaunganisha Tanzania na Malawi ambapo nchi ya Malawi inategemea sana usafiri wa Meli kwa ajili ya kusafirishia bidhaa za kutoka na kuingia nchi hiyo.

“ Mahitaji na matumizi ya wananchi ni makubwa mno na Serikali ya Mkoa inataka kuona utengenezaji wa Meli hizi unakamilika kwa wakati ili wananchi waanze kunufaika mapema na jitihada za Serikali yao”.

Kwa upande wake Meneja wa Bandari Kyela Bw. Ajuaye Msese amesema kuwa mradi wa ujenzi wa Meli unaendelea utarahisisha shughuli za kiuchumi kijamii na kiusalama kwa wanancnhi wa eneo la Bandari. Mamlaka imelenga kuifanya Bandari ya Itungi kuhudumia abiria na Mizigo mchanganyiko na ile ya Kiwira kuhudumia Mizigo kama Makaa ya Mawe, Mbolea na Saruji kama sehemu ya utekelezaji wa sheria ya Mazingira.

Bw. Msese amesema kuwa Mamlaka iko katika hatua nzuri za kuhakikisha inapata eneo katika Mkoa wa Mbeya kwa ajili ya ujenzi wa Bandari Kavu ambayo itakuwa kiungo muhimu kwa Mizigo inayosafirishwa kutoka Dar es Salaam kupitia reli ya TAZARA kwenda nchi jirani Malawi, Zambia na DRC.

Naye Mkuu wa Wilaya wa Kyela Bi. Claudia Kita ameahidi ushirikiano wa kutosha kwa Mamlaka ya Bandari katika kuzuia shughuli za kibinadamu pembezoni mwa Mito ili kuzuia mchanga kujaa katika kingo za ziwa Nyasa

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa