• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mbeya Waadhimisha Siku ya Uhuru kwa Kupanda Miti

Imetumwa : December 9th, 2020

Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini imesema kuwa itafanya ufuatiliaji wa matunzo ya miche 100 iliyopandwa katika Shule ya Msingi Magufuli Mchepuo wa Kiingereza.

Kamishna Msaidizi wa uhifadhi Kanda ,Cosmas Ndakidemi amesema leo Desemba, 9 katika maadhimisho ya siku ya uhuru na kwamba jumla ya miche 1,000 imepandwa katika wilaya za Mkoa wa Mbeya.

Ndakidemi amesema kuwa kwa leo wamepanda miti 100 katika shule ya Msingi Magufuli ikiwa ni uzinduzi wa ugawaji wa miche bure kwa wananchi lengo ni kuhakikisha mazingira ya Jiji la Mbeya na makazi ya wananchi yanatunzwa na kuwa kijani.

"Miche hii tumetoa bure na tunakaribisha mashirika taasisi kujitokeza kuchukua na kupanda lengo ni kuweka mazingira ya Jiji la Mbeya katika hali ya kijani na hadhi ya Green city kama miaka ya nyuma na kuhamasisha jamii kuitunza "amesema.

Aidha amesema kuwa pia TFS watafanya ufuatiliaji wa hali ya ukuaji wa miche kila wakati ili kuboresha mvuto wa mazingira katika shule hiyo.

Akizunguzma mara baada ya kupanda miche ya miti 100 katika Shule hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila, amewaagiza walimu wa shule hiyo kila mmoja kupanda miche ya matunda na kubandika kibao chenye utambulisho wa jina la

"Nimetoa agizo hilo kwa makusudi nahitahi mnapozungumzia afya bora na ulaji wa matunda uende kwa vitendo watoto wanapokuwa shule muda wa mapumziko Wale matunda kwa wingi ikiwa ni pamoja na mbogamboga "amesema.


Aidha kwa upande mwingine ameitaka jamii kuwa na utaratibu wa kutenga maeneo ya kilimo cha mbogamboga na matunda kwa kutambua kuwa afya ya binadamu inalinda na ulaji wa mboga na matunda .


Pia ametumia fursa hiyo kuonya wazee wanaiongiza migogoro ya ardhi wakati serikali inawekeza miradi ya Maendeleo hususan ujenzi wa shule za kisasa michepuo ya kiingereza.


"Kuna wazee hapa mjini wanaishi kwa utapeli na kupora maeneo ya wazi sasa nitanyooka na nyinyi kikubwa tumieni busara kwani maendeleo tunayoleta ni kwa ajili ya watoto wenu.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • RC DKT. HOMERA AKUTANA NA MABALOZI WA NCHI NNE AFRIKA

    May 26, 2025
  • "WAFUNDISHENI PIA ULAJI WA LISHE WATU MAOFISINI" - RC DKT. HOMERA

    May 26, 2025
  • FISTULA INATIBIKA, MATIBABU NI BURE, KARIBU UHUDUMIWE - DKT. HOMERA

    May 19, 2025
  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa