• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mfumo Mpya wa Uhasibu kuanza Kutumika Serikali za Mitaa

Imetumwa : June 6th, 2018

Mamlaka za Serikali za Mitaa Tanzania zinatarajia kuanza kutumia mfumo mmoja wa uhasibu wa usimamizi wa fedha za umma toleo la 10.2 (Epicor 10.2) utakaoanza kutumika tarehe 1 Julai, 2018 ili kusaidia mfanano katika uhasibu, utoaji taarifa na usimamizi wa fedha.       

Akizungumza katika Mafunzo ya Wahasibu na Waweka Hazina wa halmashauri za mikoa ya Mbeya, Songwe na Rukwa Mkuu wa Mfumo wa Mawasiliano PS3 Bw. Desderi Wengaa amesema kuwa uzinduzi wa mfumo huo mpya utafuatiwa na Mafunzo ya kina ya wiki tatu kwa watumishi 950 wa kada za uhasibu kutoka halmashauri 185 za Tanzania Bara.

Bw. Wengaa amesema kuwa Mafunzo hayo yataendeshwa na Ofisi ya Rais- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa pamoja na Serikali ya Marekani kupitia mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS 3) katika mikoa ya Mbeya, Dodoma, Iringa, Mtwara, Kagera na Mwanza.

Amesema kuwa moja kati ya maboresha makubwa katika mfumo mpya wa usimamizi wa fedha za umma ni kushushwa kwa mfumo hadi kwenye ngazi ya mtoa huduma ambapo matumizi yote yanayofanywa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa vituo vyake vya afya na shule yatahifadhiwa na kuwekwa wazi kwa vituo vya kutolea huduma pamoja na jamii wanayoitumikia” alisema Afisa huyo.

Bw. Wengaa amesema matoleo yaliyopita ya mfumo wa usimamizi wa fedha za umma yalijumuisha hitilafu za kiufundi ambazo zilididimiza mbinu bora za uhasibu na taratibu za usimamizi wa fedha, na kusababisha kuwepo kwa hati chafu kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Amesema kuwa mfumo wa Epicor 10.2 utaunganishwa na mfumo unaowezesha mabenki kulipana Tanzania (TISS) ambao utaruhusu malipo yote kufanyika kwa njia ya kielektroniki, pia unahusisha Muundo mpya wa uhasibu (New Chart of Account) pamoja na Kasma Mpya ya 2014 (GFS) kama ilivyoelekezwa na Wizara ya Fedha na Mipango.

Akifungua Mafunzo hayo Afias Elimu wa Mkoa Bibi Paulina Ndigeza kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa amewapongeza waandaaji wa Mafunzo kwa kufanikisha utengenezaji wa mfumo huo.

Bibi Ndigeza amesema kuwa Mafunzo hayo yana lengo la kuwajengea uwezo ili waweze kusimamia mapato na matumizi ya Fedha za Umma kwenye Halmashauri na pia kuwapatia uelewa wa mabadiliko ya msingi yalilofanyika bila kukwamisha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Ameongeza kuwa Mafunzo hayo yataondoa changamoto za utoaji wa taarifa hasa kutoka kwenye vituo vya kutolea huduma pamoja na kuunganisha Taarifa hizo kwenye Hesabu za Halmashauri, pia utatoa taarifa za utekelezaji za mipango na bajeti kwa kuzingatia matumizi ya fedha yaliyofanyika.

Bibi Ndigeza amewapongeza wataalam wote walioshiriki kufanikisha mifumo yetu ya LGRCIS (Mfumo wa Mapato), PlanRep, FFARS na Epicor kuweza kubadilishana Taarifa na kuwashukuru sana Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID) kupitia mradi wa PS3 kwa kufadhili Mafunzo.

“Sisi Makatibu Tawala wa Mikoa, ambao ni viongozi wa Mikoa tutahakikisha matumizi sahihi ya mifumo yanakuwepo ikiwemo matumizi ya taarifa katika kufanya maamuzi kuanzia ngazi za vituo vya kutoa huduma mpaka ngazi ya Mkoa” amesema Katibu Tawala.



Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa