• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mgodi wa Kiwira Kuanza Kufanya Kazi

Imetumwa : February 20th, 2018

NAIBU Waziri wa Madini,Dotto Biteko amewataka wakazi wa vijiji vilivyopo jirani na mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira wilayani hapa kuwa watulivu na kuwahakikishia kuwa mgodi huo utafufuliwa na watapata ajira kama zamani.

Mhe.Biteko alisema hayo katika nyakati tofauti alipokuwa wilayani Kyela na Ileje baada ya kutembelea mradi huo na kujionea uwekezaji uliofanyika wakati mgodi huo ulipokuwa ukifanya kazi.

Miongoni mwa maeneo ambayo naibu waziri huyo alilazimika kuzungumzia mikakati ya Serikali ni pamoja na alipokutana na wakazi wa vijiji jirani walioomba kujua hatima ya mgodi huo sambamba na maslahi ya waliokuwa wafanyakazi wakati ulipokuwa ukifanya kazi aliokutana nao wakati akitoka mgodini hapo.

Wananchi hao waliokusanyika getini waliomba Serikali kuufufua mgodi huo wakisema kutofanya kazi kwa mgodi huo kumewasababishia kuwa na hali ngumu ya kimaisha ambapo baadhi yao wamelazimika kujiingiza katika ujangili wa uchomaji mkaa hatua inayohatarisha misitu ya asili.

Hata hivyo naibu Waziri alisema nia ya Serikali ni kufufua mradi huo hivyo wakazi wa maeneo ya jirani hawana budi kuwa watulivu wakati jitihada mbalimbali zikifanyika.

Aidha Biteko aliagiza uongozi wa mgodi uliopo hivi sasa kutoaa kipaumbele kwa wakazi wa maeneo ya jirani kwa kuwapa ajira za muda zikiwemo za kufanya usafi ndani ya mgodi huo pale Serikali inapotoa fedha ili wazidi kushiriki katika kulinda mali za umma zilizopo kwenye eneo hilo wakati jitihada za kufufua mgodi zikiendelea kufanyika.

“Tunapenda mtambue kuwa huu ni moja kati ya migodi mikubwa ambayo Serikali kamwe jhaiwezi kuiacha ikafa.Kuweni na subra kama ambavyo mmekuwa watulivu kwa muda mrefu.Tuna wahakikishia hakuna aliye na haki taachwa asilipwe hapa.Na tunawahakikishi mgodi huu lazima ufufuliwe.Tungekuwa hatuna nia ya kuufufua tusingekuwa na sababu ya kuharibu mafuta ya Serikali kuja huku”

“Lakini pia nimeagiza uongozi,Serikali inaleta fedha hapa kwaajili ya shughuli ndogondogo wakati tukiendelea kufanya jitihada za kufufua mgodi.Hizi kazi wawape ninyi miliopo jirani ili walau kasungura haka kadogo na ninyi mkafaidi wakati tunaendelea na mambo mengine.Sasa sasa hata hiki kidogo tunacholeta nacho msipate,itakuwa si haki na Serikali yetu haitaki hivyo.”alisisitiza Biteko.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Kyela, Mhe Claudia Kita na mkuu wa wilaya ya Ileje Joseph Mkude walisema wakazi wa wilaya hizo mbili wana uchu wa kuona mgodi huo unafufuliwa na kuanza kufanya kazi ili waweze kunufaika nao kama ilivyokuwa awali.

 Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela, Mhe Dk Hunter Mwakifuna alisema kufufuliwa kwa mgodi huo kutapunguza changamoto ya uhaba wa ajira uliopo katika wilaya hizo mbili na kuwa Serikali nayo itanufaika kwa kiasi kikubwa hasa kutokana na uwepo wa Meli kubwa mpya katika ziwa Nyasa zitakazotumika kusafirisha makaa yam awe kwende nchi jira

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa