• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Halmashauri ya Jiji la Mbeya yapokea Magari kutoka HJF Medical Research International

Imetumwa : June 11th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Amos Makalla amekabidhi magari mawili kwa Halmashauri ya Jiji la Mbeya yenye thamani ya shilingi 191,703,073 kwa ajili ya kufanya ziara za usimamizi shirikishi na uhakiki wa ubora wa taarifa kwenye masuala ya UKIMWI.

Akikabidhi magari hayo yaliyofadhiliwa na watu wa Marekani kupitia shirika la HJF Medical Research International, Mh. Makalla alieleza furaha yake kwa Serikali ya Marekani kwa kuwa na imani na Mkoa wa Mbeya hadi kufikia hatua ya kutoa msaada katika sekta mbalimbali ikiwemo ya afya.

Mhe. Makalla alisema bajeti ya Marekani imekua ikiongezeka kila mwaka ili kufanikisha mataifa katika masuala mbalimbali ya kijamii ikiwemo utoaji wa huduma bora za afya kama ilivyo kwa Tanzania.

“ Wafadhili wametoa msaada ni lazima Wakurugenzi wasimamie  kutunza magari haya ili yaweze kusaidia na kufanya kazi iliyokusudiwa kwa ajili ya mapambano dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi,” alisema Mhe Makalla.

Naye Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Jiji Dkt. Jonas Lulandala alisema magari hayo yatasaidia sana katika ukusanyaji wa sampuli za damu kwa wakati na upelekaji katika maabala ya Kanda, kusambaza dawa na vifaa tiba kwa wakati.

Dkt Lulandala amesema kuwa halmashauri imekuwa ikifanya ziara za usimamizi shirikishi na uhakiki ubora wa taarifa mara kwa mara katika vituo vyote vya huduma ya afya, tiba na matunzo pamoja na ufuatiliaji wa ubora wa kazi kwa watoa huduma na kwendesha mafunzo kazini yaani ‘Mentorship’.

Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya Mh David Mwashilindi aliahidi kuisimamia Halmashauri yake ili kuyatumia magari hayo kama yalivyokusudiwa.

Mhe. Mwashilindi amesema kuwa Halmashauri ya Jiji la Mbeya inatekeleza mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi katika Mkoa wa Mbeya kwa kutoa elimu ya kujikinga na maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi, upimaji wa VVU, utoaji wa dawa za kupunguza makali ya virusi vya Ukimwi ARVS pamoja na upimaji wa wingi wa virusi vya ukimwi.

Mradi wa HJFMRI umetoa magari 11 kwa Ofisi ya Mkuu wa Mko wa Mbeya na Halmashauri zake kwa lengo la kuwezesha kufanya ziara za usimamizi shirikishi na uhakiki wa ubora wa Taarifa mara mara katika Vituo vyote vya huduma ya afya, tiba na matunzo na pia kwenye ukusanyaji sampuli za damu kwa wakati na upelekaji wa sampuli katika maabara ya Kanda.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa