• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Miaka 40 ya NIMR

Imetumwa : November 19th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe Albert Chalamila amewaasa watafiti, watoa huduma na wananchi kutumia kituo Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu Mbeya kutatua matatizo ya afya yanayowakabili wananchi katika Nyanda za Juu Kusini.

Mhe Chalamila ameyasema hayo leo 19 Novemba 2020, kwenye maadhimisho ya miaka 40 tangu kuanzishwa kwa Taasisi hiyo nchi Tanzania na kuwataka watoa huduma kutumia matokeo ya tafiti katika kufanya maamuzi na kuandaa mipango ya Huduma za Afya za Wilaya na Mikoa.

Amesema kuwa huu ni mfano tosha wa maboresho makubwa yanayofanywa na kituo cha Mbeya kwa kufanya kazi kubwa ya kuimarisha matokeo ya utafiti ambayo ndiyo yanatusaidia kupata tiba, dawa na chanjo bora.

“NIMR imefanikiwa kufanya tafiti muhimu sana zilizochangia kuboresha au kutoa taarifa zilizopelekea kuboresha huduma za kudhibiti UKIMWI  na magonjwa nyemelezi , magonjwa ya kitropiki yaliyokuwa hayapewi kipaumbele, Malaria, Kifua Kikuu, Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto na Saratani ya shingo ya kizazi na magonjwa yasiyoambukizwa katika maeneo ya mikoa ya Nyanda za Juu Kusini Magharibi”  Mhe. Chalamila

Aidha, Chalamila amemshukuru Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Magufuri kwa kuendelea kuboresha na kuweka mkazo katika sekta ya afya kwa kufanya uwekezaji mkubwa katika kituo chetu hiki cha Mbwya

“Nimepata muda wa kutembelea moja ya maabara ya kituo hiki na kujionea uwekezaji mkubwa uliofanywa na serikali ya Tanzania pamoja na wadau mbali mbali wa maendeleo. Maabara hii ina vifaa vya kisasa kabisa na ithibati (accreditation) ya kimataifa ambapo ziko maabara mbili tu Afrika nyingine ikiwa Uganda zenye Ithibati ya namna hii” Chalamila

Akimkaribisha Mkuu wa Mkoa Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa NIMR ambaye pia ni Mkurugenzi Mratibu wa Taarifa na Mawasiliano ya Kitafiti NIMR, Dkt Ndekya Oriyo taasisi ilizaliwa baada Serikali kuona uhitaji wa kuwa na chombo cha kisayansi kwa ajili ya utafiti na kwa sasa taasisi ina vituo vikubwa saba na vituo vidogo saba.

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt Osmunda Mwanyika ameipongeza NIMR kwa jitihada zao toka mwaka 1980 mpaka sasa za kuhakikisha afya za wananchi zinaimarika na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiano kuanzia ngazi ya halmashauri hadi mkoa.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa