• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkoa wa Mbeya wapata Matokeo Mazuri katika Elimu

Imetumwa : February 12th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Amos Makalla amewapongeza Wananchi, Wadau wa Elimu, na Walimu Mkoani Mbeya kwa kuwezesha matokeo mazuri ya Mitihani ya Kitaifa ya Kidato cha Nne na Darasa la Saba na Mitihani ya kujipima ya Kidato cha Pili na Darasa la Nne.

Ameyasema hayo katika Kikao cha Elimu ya Mkoa kilichoandaliwa kwa ajili ya kupongeza Wadau wa Elimu kwa kuwezesha Mkoa kupanda kutoka nafasi ya 13 hadi ya 6 kwa mtihani wa Kidato cha Nne na nafasi ya 22 mpaka 17 kwa matokeo ya Darasa la Saba mwaka 2017.

Amewashukuru wananchi wa Mkoa wa Mbeya kwa kuonyesha ushirikiano Mkubwa wa kutatua changamoto za Elimu Mkoa wa Mbeya hasa katika masuala ya ujenzi wa madarasa, kuweka mahusianao mazuri na walimu na kusimamia wanafunzi kwenda shule na kupunguza Idadi ya utoro mashuleni.

Mhe Makalla amesema kuwa matokeo hayo yamekuja baada ya kuandaa Kikao cha Wadau mwaka jana kuangalia jinsi ya kubadilishana mawazo na uzoefu pia kuangalia changamoto zinazoikuta sekta ya Elimu Mkoa wa Mbeya.

“Tulikubaliana suala la elimu lipewe kipaumbele kuanzia ngazi za Kijiji hadi ya Wilaya kwa kuweka iwe ajenda muhimu katika vikao mbalimbali vya maendeleo na pia kujenga mahusiano mazuri kati ya wazazi, wananafunzi na Walimu” Amesema

Mhe. Makalla amesema kuwa hataharakisha kuwavua madaraka waratibu wa Elimu au Walimu wa kuu kwa kupata matokeo mabaya kwa sababu changamoto nyingi ndani ya sekta ya Elimu zinahusisha hasa wananchi na Serikali na kusema madaraka yatavuliwa kwa Walimu na Waratibu pale tu watakaposhindwa kutimiza majukumu yao.

Dr. Tulia AcksonNaibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amemshukuru Mkoa kwa kazi nzuri inayofanyika hapa Mkoani hasa kwa kutambua juhudi za wananchi, Walimu na Wadau wa Elimu katika kuwezesha mkoa kupata matokeo mazuri katika mitihani ya Kitaifa.

Dk Ackson amesema kuwa kama mdau wa Elimu atahakikisha anashrikiana na Mkoa kuendelea kutambua juhudi za wananchi, Wadau wa Elimu na Walimu na kwa kuanza Tulia Trust imewapa zawadi ya fedha taslimu Wanafunzi waliongoza kufaulu Kimkoa na Shule zilizoongoza Kimkoa

Naye Bw. Ndele Mwaselela Mdau wa Elimu amemshukuru Mkoa kwa kutambua michango wanayoitoa katika ujenzi wa madarasa na utoaji wa Vifaa vya Elimu kwa shule za Mkoani Mbeya na kuahdid kuendelea kushirikiana na wananchi kuwezesha Mkoa kupata matokeo mazuri zaidi.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa