• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

RC azuia Zoezi la Kuhamisha Wananchi

Imetumwa : January 2nd, 2018


SERIKALI Mkoani Mbeya imesitisha kuondolewa kwa wakazi wa Kijiji cha Sipa kilichopo katika Kata ya Kambikatoto wilayani Chunya kutokana na mipaka ya eneo la Kijiji hicho kutoeleweka vema iwapo ni sehemu ya hifadhi,pori la akiba au eneo tengefu la malisho.

Hayo yamejiri zikiwa ni siku chache tangu Serikali wilayani Chunya ifanye oparesheni ya kuwaondoa wavamizi wa maeneo ya Hifadhi na mapori ya akiba wilayani hapa ambapo wakazi wa kijiji cha Sipa pia ilikuwa waondolewe kijijini hapo.

Katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini Sipa juzi,Mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na Usalama Mkoa wa Mbeya,Mkuu wa Mkoa ,Amosi Makalla aliamuru wakazi hao wapatao zaidi ya 8000 waendelee kuishi kwa amani kijijini kawao.

“Taarifa zenyewe zinajichanganya,wapo wanaosema eneo hili ni la Tanapa,wapo wanaosema ni eneo lilitengwa kwaajili ya malishio ya mifugo ya kijiji mama cha Kambikatoto na wengine wanasema ni pori la akiba.Lakini mpaka mnajenga majengo ya shule,mna mtendaji na mwenyekiti wa kijiji kwa nini leo tuseme mpo hapa kinyume cha sheria”

“Sasa ninachosema mimi kuanzia leo endeleeni kuishi kwa amani katika eneo hili ambalo mmejenga.Lakini nataka viongozi wa kijiji mama cha Kambikatoto walete mihutasari inayoeleza eneo hili lilitengwa kwaajili ya nini ili tuone nini cha kufanya”alisema Makalla.

Hata hivyo Mhe. Makalla aliwaonya watu wote waliotimuliwa kwenye maeneo ya hifadhi yakiwemo ya Mdabulo na Manyanga kutorejea tena huko kwakuwa kuondolewa kwao kuna sababu za msingi kisheria.

Awali mkuu wa wilaya ya Chunya,Rehema Madusa alisema asilimia kubwa ya wakazi wa kijiji cha Sipa ni wahalifu waliokimbia kutoka maeneo mbalimbali nchini hivyo walihamia kwenye eneo hilo kama sehemu ya kujificha lakini wakiwa hapo wamekuwa wakijishughulisha na shughuli mbalimbali za uharifu ikiwemo uwindaji haramu wa Tembo na uvunaji magogo na mbao.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa