• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkuu wa Mkoa Afungia Mgodi Chunya

Imetumwa : July 4th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. A mos Makalla, imeufunga Mgodi mmoja na kusimamisha kiwanda kimoja cha kuchenjua dhahabu wilayani Chunya kutokana na kukiuka taratibu za madini ikiwemo kutumia milipuko mikubwa inayosababisha madhara kwa wananchi.

Mgodi uliofungwa ni wa Gabriel Resources, ambao unadaiwa kusababisha madhara makubwa kwa wananchi wa Kijiji cha Mlima Njiwa katika Kata ya Mbugani kutokana na kutumia milipuko iliyosababisha kubomoka kwa nyumba za wananchi pamoja na Zahanati.

Akitangaza uamuzi wa Kuufunga Mgodi huo kwenye Mkutano wa Hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Mlima Njiwa, Mhe Makalla, alisema alipata malalamiko kutoka kwa wananchi kuwa wawekezaji hao wanasababisha madhara kwao.

Makalla alisema baada ya kupata malalamiko hayo, alifika katika kijiji hicho na kuwasikiliza wananchi pamoja na mwekezaji wa Mgodi huo ambaye alikiri kutumia milipuko hiyo ndipo akaamua kusimamisha shughuli za uchimbaji na kisha kuunda tume ya kuchunguza tuhuma hizo

“Tulipofanya mkutano hapa mlitoa ushuhuda kuhusu madhara mnayoyapata kutokana na milipuko ambayo ilikuwa inafanywa hata mchana, mlieleza namna nyumba zenu zilivyopata mipasuko na zahanati yenu kubomoka, wanafunzi wanavyopata shida shuleni,”

“Tume imebaini kuwa kweli mwekezaji huyu alikuwa anatumia milipuko mikubwa na hata baada ya mimi kusimamisha shughuli za ulipuaji wao waliendelea kulipua na kuendelea kuleta madhara kwa wananchi, sasa kuanzia sasa naufunga mgodi huu pasifanyike shughuli zozote,” alisema Makalla.

Aidha Makalla alisema waliamua kusimamisha shughuliza uchenjua dhahabu za Kiwanda kinachomilikiwa na Isack Msowoya, kilichopo katika Kijiji hicho cha Mlima Njiwa, kutokana na kujengwa kwenye eneo la chanzo cha maji na hivyo kuhatarisha maisha ya wananchi kutokana na matumizi ya kemikali.

Vilevile alisema mmiliki wa Kiwanda hicho hana kibali chochote cha kumuwezesha kuendelea na shughuli za uchenjuaji wa madini ikiwemo kibali cha Baraza la Mazingira la Taifa (Nemc), Jeshi la Zimamoto pamoja na cha Usalama mahali pa kazi (Osha).

Alisema kitendo cha mwekezaji huyo kutokuwa na vibali hivyo ni kosa kisheria na kwamba kuna uwezekano wa kemikali zinazotumika kuchanganyika kwenye maji wanayotumia wananchi.

Baadhi ya wananchi wa Kijiji hicho, waliishukuru Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa kwa uamuzi wake wa kuufunga Mgodi huo pamoja na Kiwanda kwa madai kuwa walikuwa katika hatari ya kuathirika na shughuli hizo.

Diwani wa Kata ya Mbugani, Bosco Mwanginde, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chunya, alisema uamuzi huo ni mzuri kutokana na wawekezaji hao kubainika kuwa walikuwa wanakiuka sheria za nchi.

Alisema wananchi wake walikuwa wanaathiriwa na shughuli za mgodi pamoja na kiwanda hicho na kwamba endapo shughuli hizo zingeachwa ziendelee, madhara yangekuwa makubwa zaidi.

“Pamoja na kwamba hawa watu walikuwa wanalipa kodi na kuajiri watu wetu, lakini maisha ya watu ni mhimu zaidi kwahiyo, kamati ya ulinzi na usalama imetusaidia sana,” alisema Mwanginde.

Naye Eva Daniel, alisema Serikali imewasaidia kwa madai kuwa Mgodi wa Gabriel Resources, umesababisha madhara kwao kwa kubomoa nyumba na kwamba walikuwa wanaishi kwa wasiwasi.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • RC DKT. HOMERA AKUTANA NA MABALOZI WA NCHI NNE AFRIKA

    May 26, 2025
  • "WAFUNDISHENI PIA ULAJI WA LISHE WATU MAOFISINI" - RC DKT. HOMERA

    May 26, 2025
  • FISTULA INATIBIKA, MATIBABU NI BURE, KARIBU UHUDUMIWE - DKT. HOMERA

    May 19, 2025
  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa