• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkuu wa Mkoa Atoa Siku 14 kwa Viongozi wa Wilaya

Imetumwa : May 28th, 2021

Na Nebart Msokwa, MBEYA

MKUU wa Mkoa wa Mbeya, Juma Homera amewapa siku 14 wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri zote za mkoa huo kuandaa madirisha maalumu kwa ajili ya kuhudumia wazee  kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

Alitoa agizo hilo mwishoni mwa wiki wakati wa kikao na wawakilishi wa wazee kutoka katika wilaya zote za mkoa huo kilichofanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Mbeya ambapo alisema baada ya siku hizo kumalizika atafanya ziara ya kukagua madirisha hayo kwenye vituo hivyo.

Alisema baada ya siku hizo kuisha hatataka kuona wazee wanapanga foleni kwenye vituo vya kutolea huduma za afya, kutamkiwa lugha mbaya wala kutakiwa kwenda kununua dawa kwenye maduka ya watu binafsi kwa maelezo kuwa Serikali inapeleka dawa kwa ajili ya kundi hilo kwenye vituo hivyo.

“Haiwezekani wazee wetu wamelitumikia taifa letu kwa uzalendo halafu wawe wanapata shida, sio mzee ana kitambulisho kinachomtaka atibiwe bure halafu anasimama kwenye foleni, kila muda anaambiwa subiri inaweza ikafika muda mzee akaanguka, sasa sihitaji mambo hayo,” alisema Homera.

Aidha alilitaka Jeshi la Polisi kufanya doria za mara kwa mara katika maeneo mbalimbali na kuwachukulia hatua kali vijana wote ambao hawafanyi kazi na badala yake wanacheza michezo isiyoruhusiwa kuchezwa mchana.

Alisema baadhi ya vijana hao ndio wanaofanya matukio ya unyanyasaji dhidi ya wazee ikiwemo kuwaibia, kuwapiga na hata kuwatamkia maneno machafu.

Alisema baadhi ya vijana hao huwa wanavuta bangi na kutumia dawa zingine za kulevya hali ambayo inachochea vitendo vya uharifu kwenye jamii.

Katika hatua nyingine aliwataka wakurugenzi wa halmashauri zote za mkoa huo kuhakikisha zinatenga bajeti kwa ajili ya kushirikiana na Wakala wa Barabara za mijini na vijijini (TARURA) kuboresha barabara huku akilitaka Jiji la Mbeya kutenga Sh. Bilioni moja kila mwaka.

Awali baadhi ya wazee wa Mkoa huo, waliiomba Serikali iwasaidie kuwadhibiti vijana wao kwa maelezo kuwa baadhi ya vijana hao wamekuwa wavivu wa kufanya kazi na badala yake wanashinda wakicheza kamali.

Mmoja wa wazee hao, Halima Mwakitalima kutoka katika Kata ya Ilemi, alisema baadhi ya vijana wao wanavuta bangi na kunywa pombe kali za moshi (gongo) na wakirejea nyumbani wanaanza kuwapiga wazazi wao bila hata sababu.

“Tunaomba mtusaidie maana hatuna amani kabisa, watoto wetu wanakunywa sana pombe na kuvuta mibangi na wakifika nyumbani wanaanza kutupiga na kutudhalilisha wazazi wao,” alisema Halima.

Kwa upande wake mzee Hosea Osasine kutoka katika Wilaya ya Mbarali alimuomba Mkuu wa Mkoa kuwasaidia kutatua migogoro ya ardhi katika Wilaya hiyo kwa maelezo kuwa wazee ndio wanaoathirika zaidi na migogoro hiyo.

Alisema baadhi ya migogoro inayowatesa wananchi wa Mbarali ni ya wakulima na wafugaji, wananchi na Hifadhi ya Taifa ya Ruaha pamoja na migogoro ya wakulima wadogo na wawekezaji wa mashamba makubwa.

mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa