• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkuu wa Mkoa Awataka Watumishi Kuacha Urasimu

Imetumwa : November 29th, 2019

Mbeya. Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila amesema vitendo vya urasimu na rushwa vinavyofanywa na baadhi ya watendaji Serikalini ndio sumu inayokwamisha kasi ya uwekezaji wa viwanda.

Chalamila aliyasema hayo jana wakati akikagua ujenzi wa kiwanda cha kisasa cha kusindika maziwa kinachojengwa na Kampuni ya Asas Dairies Ltd wilayani Rungwe, ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kutembelea, kuzindua miradi ya maendeleo na kzungumza na wananchi katika mikutano ya hadhara.

Alisema wawekezaji wengi wanaojitokeza kutaka kuanzisha viwanda mkoani Mbeya wanakutana na mazingira magumu ya urasimu na kuombwa rushwa na maofisa wa Serikali hali ambayo inawakatisha tama na kuamua kupeleka miradi hiyo maeneo mengine.

“Nimebaini kuwa urasimu na rushwa ndiyo sumu ambayo inakwamisha uanzishwaji wa viwanda mkoani hapa, baadhi ya watendaji mmekuwa na urasimu huku wengine mkithubutu kuomba rushwa ili mkubali kutoa maeneo au vibali vya uanzishwaji wa viwanda,” alisema Chalamila.

Alitoa mfano uwekezaji wa kiwanda cha mbegu ambao unataka kufanywa na kampuni ya Seedco ambao umekwamishwa na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kwa kutokuwa wepesi kuidhinisha eneo la ujenzi wa kiwanda hicho.

Chalamila alisema amebaini kuwa muwekezaji huyo amezungushwa kupewa kibali cha ujenzi wa kiwanda hicho mpaka akakaribia kukata tama na kutaka ahamishe kiwanda hicho kukipeleka mkoa mwingine.

Alisema baada ya kubaini suala hili amekutana na muwekezaji huyo na kumsihi asikate tamaa na kumuahidi kushughulikia changamoto hiyo na kuhakikisha anapewa kibali hicho haraka iwezekanavyo.

“Leo hii ninapozungumza kuna muwekezaji wa kiwanda cha Seedco walikuwa wanapaswa kuondoka kwenda kuanza kuwekeza mahali pengine kwa sababu waliomba ardhi kwa muda mrefu lakini mpaka muda huu tulikuwa bado hatujatoa hiyo ardhi, nimemuagiza Mkurugenzi wa Mbeya vijijini ndani ya siku tano awe amekwishatoa imvoice inayotakiwa kwa ajili ya malipo kidogo ya hiyo ardhi ili tufunge kiwanda kikubwa cha masuala ya mbegu bora kabisa hapa Tanzania,” alisema Chalamila.

Aidha Chalamila aliuagiza uongozi nwa Wilaya ya Rungwe kuanza mkakati wa kupata kiwanda cha kuchakata ndizi ili wilaya hiyo iache kusafirisha ndizi ghafi kwenda Dar es Salaam na badala yake isafirishe bidhaa zitokanazo na zao hilo.

Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Julius Chalya alisema amepokea maagizo hayo na kudai kuwa wilaya hiyo inayo mazao makuu matano ambayo tayari wamejiwekea mkakati wa kila zao kuwa na kiwanda chake kwa ajili ya usindikaji.

Chalya aliyataja mazao hayo kuwa ni chai, Parachichi, Kahawa, ndizi, maziwa na viazi mviringo.

Alisema mpaka sasa mazao matatu tayari yameshafanikiwa kupata kiwanda kwa ajili ya usindikaji na mengine mawili wanaendelea kutafuta wawekezaji watakaowekeza kwenye maeneo hayo.

“Mpaka sasa tayari tuna viwanda viwili vya kusindika chai, tunacho kiwanda cha maparachini na sasa kiwanda cha maziwa kinajengwa na kimekaribia kukamilika,” alisema Chalya.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe, Ezekiel Mwankota alisema kuwa Wilaya ya Rungwe kwa sasa inazalisha zaidi ya lita milioni 63 kwa mwaka na kwamba kiwango hicho cha maziwa kinahitaji uwekezaji mkubwa wa viwanda ili maziwa hayo yaweze kusindikwa na kupata bei nzuri.

Alisema mpaka sasa utafiti uliofanyika unaonyesha ni asilimia 11 tu ya maziwa yanayozalishwa wilayani Rungwe ndiyo yanayonunuliwa kwa ajili ya kusindikwa viwandani na mengine yanaishia kununuliwa kwa bei ndogo mitaani kwa ajili ya matumizi ya majumbani.

Alisema uwepo wa kiwanda hicho utasaidia maziwa mengi zaidi kununuliwa viwandani, jambo ambalo pia litaongeza bei ya maziwa kutoka kwa wafugaji, sambamba na kutoa ajira kwa wananchi wa Rungwe.

 Awali, Mratibu wa Kampuni ya Asas Dairies Ltd, Lipita Mtimila alimueleza Chalamila kwamba kiwanda hicho kitakamilika June mwakani na kitakuwa na uwezo wa kusindika lita 50,000 kwa muda wa masaa nane

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • RC DKT. HOMERA AKUTANA NA MABALOZI WA NCHI NNE AFRIKA

    May 26, 2025
  • "WAFUNDISHENI PIA ULAJI WA LISHE WATU MAOFISINI" - RC DKT. HOMERA

    May 26, 2025
  • FISTULA INATIBIKA, MATIBABU NI BURE, KARIBU UHUDUMIWE - DKT. HOMERA

    May 19, 2025
  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa