• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Apokea Vyumba vya Madarasa kutoka Bioland

Imetumwa : February 14th, 2018

MKUU wa Mkoa wa Mbeya,Amos Makalla amepokea vyumba viwili vya madarasa na kimoja cha Ofisi ya walimu vilivyojengwa kwa msaada mkubwa wa Kampuni inayojishughulisha na unuzuzi wa zao la Kakao wilayani Kyela ya Kim’s chocolate(Belgium) Bioland International katika Shule ya msingi Ngana iliyopo wilayani hapa.

Mhe Makalla pia amepokea madarasa vyumba viwili vya madarasa vilivyojengwa na Kampuni hiyo katika Shule ya Msingi Lubele iliyopo katika kata ya Ikimba.

Kwa mujibu wa Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela,Mwalimu Polemone Ndarugiliye ujenzi wa vyumba vitatu katika shule ya msingi Ngana ulioambatana na ukarabati wa vyumba vingine viwili shuleni hapo uligharimu Shilingi 23,271,000 ambapo kampuni ya Bioland ilichangia Shilingi 17,000,000 sawa na asilimia 73.1,wananchi Shilingi 5,128,000 sawa na asilimia 22 kupitia nguvu kazi.

Mwalimu Ndarugiliye amesema Serikali kupitia fedha za mfuko wa jimbo ilichangia shilingi 600,000 sawa na asilimia 2.6 na Shule ya Msingi Ngana kupitia fedha za ruzuku ikachangia Shilingi 534,000 sawa na asilimia 2.3.

Amesema kwa Ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika Shule ya msingi Lubele uliogharimu Jumla ya Shilingi 14,756,500 mchango wa Kampuni hiyo ni Shilingi 9,821,000,wananchi kupitia nguvu kazi Shilingi 4,352,000,Diwani Shilingi 682,000 na madhehebu mbalimbali ya dini Shilingi 201,000.

Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo,Makalla aliwataka wakazi wilayani hapa kuendelea kushirikiana kwa karibu na Kampuni hiyo kwakuwa inaonyesha jitihada nzuri za kuboresha miundombinu ya Elimu.

Kwa upande wake Afisa kutoka Kampuni ya Bioland,Fons Maex amesema kampuni bado ina utayari wa kuendelea kusaidia ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya elimu katika Shule zote za msingi zilizopo kwenye Halmashauri za Kyela,Rungwe na Busokelo.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa