• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

RC Chalamila Anusa Ufisadi Halmashauri ya Jiji la Mbeya

Imetumwa : August 21st, 2018

Na Nebart Msokwa, MBEYA

TATIZO la Jiji la Mbeya kushika mkia kwenye ukusanyaji wa mapato, limeendelea kushikiwa bango ambapo Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila amesema amebaini kuwa mapato yanavuja kutokana na baadhi ya watumishi wa jiji hilo kutokuwa waadilifu.

Akizungumza na watumishi wa Jiji hilo jana, Chalamila alisema amebaini kuwa baadhi ya watumishi wanamiliki vibanda vya biashara kwenye masoko mbalimbali lakini wanakwepa kulipa kodi halali za serikali.

Alisema kitendo hicho kinapelekea mapato ya serikali kupotea huku watumishi hao wakijinufaisha kwa kukusanya mapato hayo, hivyo akasisitiza kuwa bila kurekebisha hali hiyo, mapato yataendelea kupotea.

Alisema anaendelea na uchunguzi kwa kutumia vyombo vyake ili kuwabaini watumishi wote wanaomiliki vibanda kwenye masoko hayo na kwamba baada ya hapo hatua zitaanza kuchukuliwa.

“Jiji lina vyanzo vingi vya mapato yakiwemo masoko, lakini ukienda kwenye vibanda vya masoko yetu unakutana na majina ya viongozi, kwenye vibanda hivyo serikali inapata mapato sifuri halafu wenyewe wanapata asilimia nne, hatuwezi kufika,” alisema Chalamila.

Aliwataka viongozi wa Jiji hilo kufanya kazi kwa weledi bila kuingiliana majukumu ili kuinua uchumi ikiwa ni pamoja na kusaidiana kuziba mianya ya mapato kuvuja.

Aliongeza kuwa ajenda ya ukusanyaji wa mapato imeanzishwa na rais Dk. John Magufuli hivyo kila mtu anatakiwa asimamie eneo lake ili kuhakikisha mapato yanakusanywa sawasawa kwa ajili ya kuimarisha huduma za kijamii.

Hata hivyo alisema katika uchunguzi wake ameshawabaini watumishi wanne wa Jiji hilo waliojimilikisha vibanda hivyo vya serikali na kwamba anaendelea na zoezi hilo.

“Kufanya biashara kwenye vibanda vya serikali inaruhusiwa, lakini kutumia vibanda vya serikali kujinufaisha hairuhusiwi, sasa nawahakikishia kuwa nikimaliza uchunguzi nitaanza kuita mmoja mmoja kwa ajili ya mahojiano na hatua zaidi,” alisisitiza Chalamila.

Chalamila alisema uhuni kama huo ulikuwa unafanyika pia kwenye Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kabla tatizo hilo halijathibitiwa na serikali.

Alisema kuna baadhi ya watumishi wamekuwa wakiwaomba fedha watunza hazina wa halmashauri na kwamba wakiwakatalia wanaanza kuwachafua kwa kutumia itikadi za kisiasa za CCM na Chadema.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • RC DKT. HOMERA AKUTANA NA MABALOZI WA NCHI NNE AFRIKA

    May 26, 2025
  • "WAFUNDISHENI PIA ULAJI WA LISHE WATU MAOFISINI" - RC DKT. HOMERA

    May 26, 2025
  • FISTULA INATIBIKA, MATIBABU NI BURE, KARIBU UHUDUMIWE - DKT. HOMERA

    May 19, 2025
  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa