• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Sekondari ya Matundasi Kufunguliwa

Imetumwa : April 13th, 2018

Serikali Mkoani Mbeya imewahamisha wananfunzi 86 wa kidato cha kwanza waliokuwa wanasoma shule ya Sekondari ya Mkola Kata ya Makongorosi kwenda shule ya Matundasi kuanzia tarehe 23 Aprili, 2018 baada ya kuridhishwa na kukamilika kwa ujenzi wa shule hiyo kupitia nguvu za wananchi

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Amos Makalla jana alipokuwa anakagua sekondari hiyo baada ya kupokea malalamiko mengi ya wazazina wananchi wa Kata ya Matundasi kutokana na kutofunguliwa shule hiyo.

Alisema amelazimika kufika kujiridhisha na ujenzi na kwamba akiwa kama kiongozi ni jukumu lake kufanya maamuzi magumu ili kujenga mahusiano mazuri baini ya Serikali na wananchi.

"Nimefika kujiridhisha kimsingi mnyonge mnyongeni haki yake mpeni kwa kweli mmefanya kitu kizuri sana sasa kikubwa muendelee kuchangia ili kuongeza idadi ya vyumba vya madarasa ili viweze kukithi mahitaji
kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha nne"alisema.

Diwani wa kata ya Matundasi Bw Kimo Choga (CCM) alisema kwa kipindi cha miaka nane sasa tangu shule hiyo ikamilike wamekuwa wakifuatilia wilayani kuomba ifunguliwe ambapo wamekuwa wakielezwa sababu zisizo za msingi jambo ambalo lilikuwa likiwakatisha tamaa wananchi.

Mhe Diwani amemwambia Mkuu wa Mkoa kuwa ujenzi ulikamilika mwaka 2011 ambapo mpaka sasa ni miaka 8 haijafunguliwa na kuomba ujio wake uwe chachu ya kutokomeza siasa inayoletwa na Viongozi wa wilaya hiyo.

Choga amesema kuwa kutaondokana na changamoto ya kutembea umbali mrefu wa kilometa 25 kufuata elimu  na  kuwasogezea uwezo kupata elimu kwa karibu bora itakayozalisha wasomi wa kizazi kijacho.

Mkaguzi mkuu na mthibiti wa ubora wa shule Kanda ya Nyanda za Juu  Kusini Merchant Mtandika, alisema shule hiyo imekidhi vigezo vinavyohitajika na kwamba kwa sasa atashughulikia usajili wakati wanafunzi wakiendelea na masomo.

Mkazi wa Matundasi Mariam Gabriel alipongeza maamuzi ya Mkoa kwani kama wananchi walishangazwa kwa kutofunguliwa kwa shule hiyo ambao imekidhi vigezo kama miundombinu ya vyumba vya madarasa,maabara ya kisasa,matundu ya vyoo jengo la utawala na ofisi za walimu.

Awali April 11 mwaka huu wanafunzi wa kidato cha kwanza shule ya sekondari Mkola waligoma kuendelea na masomo wakishinikiza serikali ya wilaya kufungua shule ya kata ya Matundasi ili kuwaondoka katika

changamoto ya kutembea umbali mrefu kufuata elimu

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa