• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Waziri TAMISEMI Awaonya Watendaji TARURA

Imetumwa : January 8th, 2018

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Suleiman Jaffo amewaonya Mameneja na Wanasheria wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini(TARURA) nchini kuacha kufanya kazi kwa mazoea badala yake wazingatie maadili ya kazi waliyopewa.

Mhe.Jaffo ametoa agizo hilo leo jijini Mbeya,alipofunguaSemina ya Siku tano ya Watendaji wa Tarura kutoka mikoa saba iliyopo Kanda ya nyanda za juu kusini.

Ameitaja Rushwa kuwa miongoni mwa mambo makubwa ambayo yamekuwa yakisababisha Zabuni nyingi kutotekelezwa kwa kufuata mikataba na kuisababishia hasara Serikali.

Amewataja wanasheria wa Serikali kuchangia kuipa Hasara Serikali kwa kushindwa kusimamia Sheria hususani kesi za wazabuni zinazopelekwa mahakamani hatua aliyosema inatokana na wau wa kada hiyo kula sahani moja na wakandarasi.

Amesema wakandarasi wengi wamekuwa wakishindwa kutekeleza kazi kwa mujibu wa mkataba na kuzusha mivutano ambayo mwishowe hufikia hatua ya kufungua kesi mahakamani lakini ajabu ni kuwa Serikali imekuwa ikishindwa kesi hizo na kulazimika kuingia hasara kwa kulipa fidia.

Waziri huyo pia amewataka mameneja wa Tarura kutambua kuwa yeyote atakayeshindwa kutekeleza majukumu yake atambue kuwa hatoweza kufika mwezi wa saba mwaka huu akiwa kwenye nafasi hiyo.

Amesema Tarura inategemewa na Taifa katika kuleta mabadiliko makubwa hasa katika kuelekea uchumi wa kati unaotegemea viwanda ambapo hauwezi kufikiwa pasipo uwepo wa miundombinu ya barabara iliyo bora.

Amesisitiza kuwa miundombinu bora itawaondolea wakulima adha ya kusafirisha mazao kutoka mashambani hadi yaliko masoko hivyo kurahisisha upatikanaji wa malighafi za viwanda

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Amos Makalla ameahidi kuendelea kusimamia kwa karibu miradi yote itakayotekelezwa na wakala huo huku akisisitiza kuwa hakuna atakaeachwa salama iwapo atabaini matumizi mabovu ya fedha za umma.

Mhe. Makalla amesema wananchi hususani wa maeneo ya pembezoni wana matarajio makubwa na Tarura hali inyotokana na adha iliyowakabili kwa miaka mingi ya ukosefu wa miundombinu rafiki ya barabara.


Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa