• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

TANROADS Yaamua Kuendelea na Ujenzi wa Barabara ya Kikusya-Ipinda-Matema

Imetumwa : March 15th, 2018

SERIKALI kupitia Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Mbeya, imeamua kuendelea na ujenzi wa barabara ya Kikusya – Ipinda – Matema katika Wilaya ya Kyela, licha ya baadhi ya wakazi wa Mji wa Ipinda kufungua kesi mahakamani kupinga nyumba zao kubomolewa.

Akitoa taarifa ya ujenzi wa barabara hiyo kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos Makalla, msimamizi wa mradi huo kutoka katika Kitengo cha ushauri wa kihandisi TANROADS (TECU), Mhandisi Samwel Mwambungu, alisema kitendo cha wananchi hao kufungua kesi kimesababisha mradi kuchelewa kukamilika.

Mhandisi Mwambungu amesema kutokana na umuhimu wa barabara hiyo kwa wananchi wa maeneo hayo, wameamua kuendelea na ujenzi kutokana na eneo lililopo huku nyumba za wananchi hao zikiachwa kama zilivyo.

Mhandisi Mwambungu, amesema barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 34.6 inajengwa kwa kiwango cha lami na Mkandarasi China New Era International Engineering Corporation kwa gharama ya shilingi milioni 56.9 na kwamba mradi unatekelezwa na serikali kwa asilimia 100.

“Mradi ulianza kutekelezwa julai 31, 2015 na ulitakiwa kukamilika ndani ya miezi 24, lakini mpaka sasa haujakamilika kutokana na baadhi ya changamoto ikiwemo baadhi ya wananchi kufungua kesi mahakamani wakipinga kupisha upanuzi,” alisema Mhandisi Mwambungu.

“Tumeamua tuendelee na ujenzi lakini kwenye eneo ambalo hawa wananchi wamegoma, tunajenga kulingana na eneo lililopo bila kugusa nyumba zao,”

Vilevile alisema Mkandarasi wakati mwingine huwa anakwama kutokana na Serikali kumcheleweshea malipo yake, kwa maelezo kuwa mpaka sasa amelipwa shilingi bilioni 7.2 kati ya bilioni 26 anazodai kulingana na kazi aliyoifanya.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Amos Makalla, ameshangazwa na kitendo cha wananchi hao kuishtaki Serikali kwa madai kuwa barabara hiyo ni faida yao wenyewe na hivyo walichokifanya wanajiumiza wenyewe.

Mhe. Makalla amesema barabara hiyo ikikamilika itafungua fursa nyingi kwao ikiwemo kurahisisha usafiri na usafirishaji wa mizigo kutoka katika maeneo yao na kupeleka maeneo ya masoko ikiwemo kupeleka Kyela mjini na Mbeya.

Aidha Mhe Makalla amesema barabara hiyo itafungua fursa kwenye sekta ya utalii kwa madai kuwa fukwe za Ziwa Nyasa katika eneo la Matema ni kivutio kikubwa cha watalii hivyo wananchi hao watanufaika kwa kuwaongoza watalii na kuwauzia bidhaa mbalimbali wanazozalisha.

“Mtunze kumbukumbu vizuri kwa kile mlichokifanya hapa, watoto wenu na wajukuu watakapowauliza kwanini barabara nyembamba hapa, mkawambie tuliipeleka serikali mahakamani ndio maana ikaamua kujenga hivyo,” alisema Makalla.

Hata hivyo Makalla amesema anakusudia kwenda kuonana na Waziri wa Ujenzi Prof. Makame Mbarawa ili kushawishi Mkandarasi wa barabara hiyo aendelee kulipwa fedha za mradi huo pamoja na kumuomba aidhinishe kipande kinachobakia kuanzia Tenende kwenda Kyela kiunganishwe kwenye Mkataba.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Claudia Kitta, aliishukuru Serikali kwa kuamua kujenga barabara hiyo akidai kuwa itakuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo.

Alisema ni nadra barabara ya kiwango kama inayojengwa katika eneo hilo kutoka mjini kwenda kijijini, hivyo akawataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Mkandarasi.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa