• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

TRA Watakiwa Kuwakagua Mawakala wa Saruji

Imetumwa : November 13th, 2020

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Mbeya imeagizwa kuanza kukagua risiti za manunuzi ya saruji kwa mawakala wa kiwanda cha saruji Mbeya katika kipindi cha wiki mbili zilizopita ili kubaini chanzo cha mfumuko wa bei ya bidhaa hiyo.

Agizo hilo limetolewa na mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila leo Ijumaa Novemba 13, 2020 baada ya kufanya ziara ya katika kiwanda cha Saruji Songwe hicho kilichopo Wilaya ya Mbeya Vijijini.

Chalamila amefika kiwandani hapo na kushuhudia wafanyakazi wakiendelea na uzalishaji na magari yakiwa kwenye foleni za kupakia saruji kwa ajili ya kusafirisha kwenda mikoani mbalimbali.

Akizungumza na uongozi wa kiwanda hicho, Chalamila amesema lengo la ziara yake ni kutaka kujua sababu ya mfumuko wa bei kama umeanzia kiwandani au la.

"Nimefika hapa ni kutokana na hali ilivyo mitaani kwa watumiaji wa saruji kwani gharama imepanda kwa kasi sana. Nikiwa kama kiongozi wa Mkoa nimelazimika kufika kujua hali halisi,” amesema.

Amesema tayari amejiridhisha kuwa chanzo sio wawekezaji bali ni mawakala, “sasa ni vyema TRA kufuatilia kuwabaini ili hatua za kisheria zianze kuchukuliwa. Nashangaa mitaani kwenye maduka saruji inauzwa kati ya Sh22,000 wakati hapa kiwandani pamoja na VAT inauzwa Sh14,500 jambo ambalo linawanyonya wananchi wa kipato cha chini.”

Mkuu huyo wa Mkoa amesema ameandika barua wizara ya viwanda kuomba kifanyike kikao cha pamoja kati ya mawakala wa usafirishaji na wawekezaji wa viwanda vya saruji.

Meneja uzalishaji wa kiwanda hicho, Godwsten Mende amesema kiwanda hakijaongeza bei ya saruji sokoni, ongezeko limetokana na uhitaji mkubwa wa watumiaji na awali baada ya kupata taarifa za baadhi ya viwanda kusitisha uzalishaji wao waliongeza uzalishaji ili kukidhi mahitaji ya wakazi wa Mbeya.

Amebainisha kuwa changamoto kubwa ni usafirishaji wa saruji kutoka kiwandani kwenda kwa mawakala  mawakala ambao wanafidia gharama za usafirishaji kwa kupandisha bei ya bidhaa hiyo.

Bw. Gembe ameiomba Serikali kuboresha usafiri wa reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) kwa kuongeza idadi ya vichwa vya treni za mizigo ili iwe fursa kwa kiwanda hicho kuwafikia wateja mikoani.

Mkazi wa Uhindini Mbeya, James Joram amekifananisha kitendo cha wafanyabiashara kupandisha bei ya saruji na uhujumu uchumi na kuitaka Serikali kusaka mwarobaini ili kuwawajibisha.

Fundi ujenzi Oscar Mwaifwani amesema awali walikuwa wakinunua mfuko wa saruji kwa Sh16,000 mpaka Sh17,000 lakini kwa kipindi cha wiki mbili imepanda mpaka kufikia Sh22,000 mpaka Sh24,000 kwa mfuko.

"Hii ni changamoto kwetu mafundi na tunaoshika tenda kubwa za miradi ya ujenzi kwani tayari tulikuwa tumepiga hesabu za manunuzi ya vifaa na inapotokea bei imepaa ni shida,” amesema.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • RC DKT. HOMERA AKUTANA NA MABALOZI WA NCHI NNE AFRIKA

    May 26, 2025
  • "WAFUNDISHENI PIA ULAJI WA LISHE WATU MAOFISINI" - RC DKT. HOMERA

    May 26, 2025
  • FISTULA INATIBIKA, MATIBABU NI BURE, KARIBU UHUDUMIWE - DKT. HOMERA

    May 19, 2025
  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa