• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Usuluhishi wa Mgogoro wa Ardhi kati ya Wananchi wa Kijiji cha Nanyara na Kiwanda cha Songwe

Imetumwa : November 2nd, 2019

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi  

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli aliagiza Wizara za Ardhi, Madini, Tamisemi na Viwanda zishughulikie mgogoro wa Ardhi baina ya Kijiji cha Nanyala na kiwanda cha Saruji cha Mbeya.

Mgogoro unahusisha ekari 2315 ambapo ekari 1475 zipo Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe na ekari 840 ziko wilaya ya Mbeya.

Leo tumekuja kama alivyoagizwa kujionea hali halisi ikiwa lengo letu ni kuumaliza mgogoro huo na tutafuata sheria taratibu na kanuni zote katika kutatua mgogoro huu.

Kufikia Jumatatu Kiwanda cha Saruji kiondoe kesi tatu zilizoko mahakamani baina ya kiwanda na wana kijiji cha Nanyala kama alivyo agiza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, hii si hiyari, haiwezekani Mkuu wa Nchi anaagiza jambo halafu kuna mtu anajivuta kutekeleza.

Utoaji wa leseni za madini katika eneo lenye mgogoro usitishwe, Kijiji cha Nanyala, Wilaya za Mbozi na Mbeya zisitishe utoaji wa hati za kimila katika eneo lenye mgogoro.

Wakulima na wafugaji ambao wanalima na kufuga katika eneo hilo, mgogoro huu hauna maslahi nao hivyo wasizuiliwe kuendelea na shughuli za kilimo na ufugaji.

Wachimbaji wadogo wadogo wa chokaa wanaofanya shughuli zao kwa msimu katika eneo lenye mgogoro wasizuiliwe waendelee kufanya kazi zao.

Naibu Waziri Madini Stanslaus Nyongo

Wataalamu waangalie namna ya kubalidisha Sheria ya Service Levy ili halmashauri za Mbeya na Mbozi waweze kufaidika kwa pamoja na sio halmashauri moja kufaidika huku nyingine ikipunjwa.

Kiwanda cha Saruji cha Mbeya kama wanataka kutunza eneo kwa ajili ya matumizi ya baadaye waangalie namna bora inayotambulika kisheria na sio kukwepa gharama kwa kutofuata taratibu na sheria.

Naibu Waziri OR TAMISEMI Josephat Kandenge

Halmashauri ambayo haikupata service levy na ilistahili kupata ilipwe kwakuwa tusirekebishe ya mbele bila kuangalia stahiki zilizopita za Halmashauri hizi.

Naibu Waziri Viwanda na Biashara Mhandisi Stella Manyanya

Wizara ya Viwanda na Biashara ingependa kuona mgogoro huu unaisha kwakuwa kiwanda cha Saruji na vingine vilivyopo katika eneo hilo vina mchango katika maendeleo ya taifa.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila

Migogoro inapoendelea sana lazima kuna upande unakuwa hauna uelewa hivyo wataalamu watusaidie katika hilo pia tusiingie sana katika mgogoro wa mapato kuwa yaende kwa nani isipokuwa tujielekeze kuumaliza mgogoro huo.

Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. Nicodemus Mwangela

Mkoa wa Songwe tunaomba kesi zifutwe ili wananchi waendelee kufanya shughuli zao kwa uhuru.

Mkoa wa Songwe tunataka wawekezaji na tunawakaribisha waje kwakuwa sisi tuna mali ghafi za kutosha ila tu wajue kuwa lazima sheria na taratibu zifuatwe.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa