• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Waumini wa Kiislamu Watakiwa Kushirikiana

Imetumwa : April 28th, 2021

NA DENIS MLOWE, KYELA

MKUU wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila amewataka waumini wa dini ya Kiislamu wilaya ya Kyela kufanya kazi kwa ushirikiano ili kukamilisha ujenzi wa msikiti wa Kalumbulu ulioanzwa kujengwa katika kata ya Mikoroshini wilayani humo mkoani Mbeya.

Akizungumza katika ziara aliyofanya wilayani Kyela, Chalamila alisema mtu wa kwanza kuwaza kutoa mchango wa ujenzi wa msikiti wa Kalumbulu alikuwa ni hayati Dk. John Pombe Magufuli ambaye alisema ujenzi wa msikiti huo atausimamia.

Chalamila alisema Mwezi wa tatu baada ya kuhudhuria kusaini mkataba wa Uganda na Tanzania hayati Magufuli aliahidi kuanza ziara katika mkoa wa Mbeya na kuahidi baada ya kukamilika kwa ujenzi wa msikiti huo ni akabidhiwe ili yeye aukabidhi kwa wananchi.

Aliongeza kuwa ni kweli hayati Magufuli amefariki imani yake alikuwa ni mkristo na sasa tunaongonzwa na rais samia suluhu hasani imani yake ni muislamu pindi atakavyoanza kufanya ziara yake hapa wilayani kyela akute msikiti huo umekamilika.

Alisema moja ya ajenda yake ni kutaka msikiti huo ukamilike hivyo amewataka waumini hao kujinyima na kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuweza kukamilika haraka kwa ujenzi wa msikiti huo .

Chalamila alisema kuwa kukamilika kwa ujenzi wa msikiti huo ni kumbukizi nzuri ya kumuenzi aliyekuwa rais wa awamu ya tano hayati Dr John Magufuli na kuwashukuru wananchi pamoja na kutoa mchango wa kiasi cha shilingi million moja ili kuchangia ujenzi wa msikiti huo wa Kalumbulu.

Hadi kufikia hatua hiyo Chalamila amekwisha changia kiasi cha shilingi milioni 15 kuweza kukamilisha ujenzi wa msikiti huo ambapo kwa sasa bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali za vifaa vya ujenzi.

 Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Kyela, Claudia Kita alisema wao kama viongozi wanaendelea kushirikiana na uongozi wa dini ya Kiislamu na kamati ya ujenzi ili kuweza kukamilisha ujenzi msikiti huo.

Kita amebainisha kuwa licha ya kuondoka kwa aliyekuwa rais wa awamu ya tano hayati Dr John Pombe Magufuli na kuacha ujenzi huo wa msikiti ukiendelea hautasitishwa na badala yake utaendelea kujengwa mpaka kukamilika kwake.

Alisema kuwa licha ya kuwepo kwa changamoto mbalimbali katika kipindi hiki cha mvua lakini hawatakata tamaa na kazi lazima iendelee ili msikiti huo uweze kukamilika.

Hata hivyo mkuu wa wilaya amemshukuru mkuu wa mkoa Albert Chalamila kwa kutoa mchango wa kiasi cha shilingi million moja ili ujenzi wa msikiti huo uweze kukamilika kwa haraka.

Naye Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa msikiti huo, Sheikhe Yusuph Tutupa licha ya kushukuru msaada uliotolewa na mkuu wa mkoa wa Mbeya alisema kuwa ujenzi wa msikiti huo unatarajia kugharimu zaidi sh milioni 200 ambapo hadi sasa uko kwa asilimia 40 ya ujenzi.

Aidha ametoa wito kwa wadau mbalimbali kusaidia ujenzi wa msikiti huo ili ukamilike kwani ni moja ya nguzo ya kutoa sadaka kwa ajili ya kupata eneo la kuabudia.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa