• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Huduma ya Kilimo

TAARIFA YA  USIMAMIZI MIRADI YA MAENDELEO

  • MIRADI MAALUM YA SEKTA YA KILIMO

Katika mwaka 2017/2018 Mkoa wa Mbeya unayotekeleza Mpango wa kuendeleza Kilimo Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (SAGGOT), Mpango wa kuendeleza kilimo cha zao la korosho na Programu ya kuendeleza mazao ya Bustani. Katika msimu wa 2017/2018 Wilaya za Kyela, Chunya na Mbarali  zimeotesha miche 132,440 ya korosho itakayopandwa katika eneo la hekta 1,892. Mkoa umepata kilo 946 za mbegu Korosho viriba vyeusi kilo 249 na matandazo kilo 78 kwa lengo hilo. Katika kuendeleza mazao ya bustani Mkoa kwa kushirikiana na TAHA na wadau wengine umefanikiwa kuunda vikundi 60 vyenye jumla ya  wakulima 2,267  waliopatiwa mafunzo ya mbinu bora za uizalishaji, masoko na lishe.

1.1 Umwagiliaji

Mkoa unaendelea kuboresha miundombinu ya umwagiliaji ili kuongeza tija na matumizi bora ya rasilimali za maji. Mkoa una hekta 110,721 zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji. Jumla ya hekta 51,046 zinamwagiliwa ikiwemo hekta 25,626 zilizoboreshwa na hekta 25,420 za asili. Aidha, katika kipindi cha 2016/2017 uboreshaji wa miundombinu uliendelea kufanyika kwenye skimu 6 katika Halmashauri ya Wilayani Mbarali (5) na Halmashauri ya Mbeya (1) kwa gharama ya shilingi 1,822,916,863. Hali ya utekelezaji wa miradi hiyo imeoneshwa katika Jedwali 1. 

Jedwali Na.1: Hali ya Miradi ya Umwagiliaji

Na.

Jina la Mradi

Jina la Mkandarasi

Lengo la Mradi

Gharama ya Mradi (Sh)

Kazi Zilizofanyika

1

Ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji Gwiri
Fair Classy Construction Ltd, S.L.P 5003, Morogoro kwa Mkataba Na. LGA/076/W/2016-2017/14
Ujenzi wa daraja na nguzo za mageti kwenye banio, vikamata mchanga 2,  na Usakafia wa mifereji ya kati mita 350

249,028,085.00

Ujenzi wa daraja na nguzo za mageti kwenye banio, vikamata mchanga 2, na Usakafia wa mifereji mita 240 (Mfereji Mkuu mita 47 na Mfereji wa kati mita 193)

2

Ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji Uturo
 IRA General Enterprise Co. Ltd S.L.P. 852, Mbeya kwa Mkataba LGA/076/W/2015-2016/13
Ujenzi wa mfereji mkuu mita 600

199,042,388.20

Ujenzi wa mfereji mkuu mita 600

3

Ujenzi wa Skimu za Umwagiliaji Uturo na Ukwavila
Classical Engineering Co. Ltd  wa  S.L.P. 4204 Mbeya kwa Mkataba Na. LGA/076/W/2015-2016/67
Kusakafia mfereji mkuu mita 500 wa skimu ya Uturo, na Ujenzi wa makalvati 15 kwenye barabara ya skimu ya Ukwavila.

145,022,000.00

Kusakafia mfereji mkuu mita 500 skimu ya Uturo, na  ujenzi wa makalvati inaendelea.

4

Ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji Mwendamtitu
DryWall Building Construction Co. Ltd na JV APE Engineering Service Co. Lld S.L.P. 240, Iringa kwa Mkataba LGA/076/W/2015-2016/11
Ujenzi wa daraja na nguzo za mageti kwenye banio, Kichuja mchaga, Kuta za gabion, makalvati, Vigawa maji na vifolu,  Tuta la mfereji mkuu na Usakafia wa mfereji mkuu mita 400

729,903,750.00

Ujenzi wa  Kichuja mchaga, Kuta za gabion, Vigawa maji,  Tuta la mfereji mkuu na Usakafia wa mfereji mkuu mita 400

5

Ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji Igomelo
Ms.KATAGAITO TRADERS CO. LTD, S.L.P. 735, TUKUYU- MBEYA kwa mkataba Na. LGA/076/W/2016-2017/12
Ukarabati wa banio na Usakafiaji wa mfereji mkuu mita 730

249,920,639.36

Usakafiaji wa mfereji mkuu mita 1,345

6

Ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji Mshewe
HAFRI TECH (T) LTD
Kusakafia  mfereji  mkuu mita 1250 na mfereji wa upili mita 400

250,000,000.00

Usakafiaji mfereji mkuu mita 200 na mfereji wa upili mita 400. Kazi iatakamilika mwishoni mwa mwezi Agosti, 2017

JUMLA KUU

1,822,916,863

 

 Chanzo: Halmashauri ya Mbarali na Mbeya, 2018

1.2 Maghala

Jumla ya maghala 13 (Ilembo, Izyira, Ihombe, Idimi, Iwowo, Mlowo, Mbagala, Izumbwe, Igale, Njelenje, Isangala, Iwiji na Pashungu) katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya yalikarabatiwa chini ya Mfumo wa Stakabadhi ya Mazao Ghalani kwa zao la mahindi kwa gharama ya Shilingi 1,467,094,175.00. Ukarabati wa maghala haya umefikia wastani wa asilimia 96.

Katika skimu za umwagiliaji Mkoa ulilenga kujenga maghala 7 (Mbarali 5 na Kyela 2) kwa gharama ya shilingi 5,714,622,821.64. Maghala yote yamekamilika. Mpango wa Mkoa wa ujenzi/ukarabati wa maghala unalenga kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna na kuwaunganisha wakulima na mifumo ya masoko

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa