• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Halmashauri Zatakiwa Kufanya Ukaguzi wa Mara kwa Mara

Imetumwa : December 12th, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Amos Makalla amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote wahakikishe kwamba maduka ya vyakula, dawa, vipodozi, machinjio zote, maduka ya nyama na samaki, migahawa na magari ya kubebea bidhaa hizi yakaguliwe mara kwa mara na hatua stahiki za kisheria zichukuliwe.

Mhe Makalla ameyasema hayo alipokuwa anafungua kikao cha Watendaji wa Mkoa na Halmashauri zote kuhusu uimarishaji wa utekelezaji wa majukumu ya TFDA yaliyokasimiwa kwa Halmashauri za Mkoa wa Mbeya kwenye Ukumbi wa Mkapa

Mhe Makalla Halmashauri zote hazifanyi kwa ufasaha kaguzi za mara kwa mara katika maduka mbalimbali ya bidhaa hizi, au vituo vya kutolea huduma, machinjio, maduka ya nyama na samaki na magari ya kubebea bidhaa hizi. Ninayo taarifa kuwa katika mkoa wetu ni machinjio MBILI ndizo zilizosajiliwa na TFDA.

Mhe. Makalla Tusitegemee mabadiliko kama tutaendelea kufanya kazi kwa mazoea. Ni budi tutambue kutambua lengo zuri la serikali la kupeleka madaraka zaidi ya utekelezaji wa majukumu ya TFDA kwa Halmashuri kuwa ni kuimarisha ufanisi wa udhibiti wa bidhaa husika. Ni vema kila mmoja akafanya sehemu yake kwa uweledi ili kuitendea haki taaluma yake na dhamana aliyopewa na jamii.

”Ninazo taarifa kwamba, makusanyo ya ada na tozo kwa huduma zilizokasimiwa, zitakusanywa ,zitabaki na kutumiwa 100% na Halmashauri.Hivyo ni kiasi cha kujua maoteo kiasi gani kinakusanya na kuingizwa katika mipango na bajeti za Halmashauri na mkoa pia ufuatilia mipango na bajeti za Halmashauri kama zinaonesha hili” . Mhe. Makalla

Mhe Makalla amesema kuwa wale wananchi au wafanyabiasha wanaofanya kwa makusudi biashara inayohatarisha afya za watanzania  hata wale wanaosafirisha bidhaa zisizofaa kwa kificho katika magari ya mizigo  au mabasi wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria na vyombo vya udhibiti na vya dola.

Mhe Mkuu wa Mkoa amesema Naamini TFDA na Halmashauri na vyombo vingine vya udhibiti mtashirikiana sana katika suala hili muhimu ikiwa pamoja na  kutoa elimu zaidi kwa wananchi ili waweze kutambua kwa urahisi bidhaa zisizofaa na kwa wafanyabiashara ili waweze kutii sheria bila shuruti.

Meneja wa   Mamlaka ya Chakula Kanda ya Nyanda za Juu  Kusini Bw Rodney Alananga amesema kuwa Halmashauri nyingi hazina takwimu kamili za majengo ya biashara za vyakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba. Halmashauri zetu pia zimekuwa zinasajili kwa kasi ndogo au hazisajili kabisa majengo yanayojihusisha na bidhaa zinazodhibitiwa na TFDA.

Bw. Alananga hadi sasa majengo ya chakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba 1,511 ( 53%) kati ya 2851  yamesajiliwa na TFDA.   Kati ya hayo yaliyosajiliwa, viwanda vya vyakula na vipodozi ni 55 ( vikubwa 19, vya kati 19 na vidogo17) .

Bw. Alananga Kazi kubwa bado ipo kwa viwanda vidogovidogo( micro) na vidogo(small) bado ambavyo vingi havijasajiliwa na tayari zipo juhudi kadhaa zimefanyika hasa kutoa elimu katika masuala mbalimbali ikiwemo ya usajili wa majengo na kanuni za usafi kwa mujibu wa sheria ya chakula, dawa na vipodozi Sura 219 uratibu ulioratibiwa na ofisi yangu ya Mkuu wa mkoa na taasisi mbalimbali za binafasi na serikali ikiwemo GS1, TFDA,TBS,SIDO,BRELA na wengine.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa