• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Halmashauri ya Kyela Yapewa Siku 3 Kumaliza Mgogoro

Imetumwa : March 13th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Amos Makalla ametoa siku tatu kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kyela na Kampuni ya IRA General Enterprises Co. Limited kufanya mazungumzo na kumaliza mgogoro baina ya pande hizo mbili ili kukamilisha mradi wa maji wa Kapapa-Butusyo uliotelekezwa kutokana na kutokuwepo na mahusiano mazuri baini ya pande hizo mbili.

Mheshimiwa Makalla ametoa agizo alipokuwa anasikiliza kero za wananchi kupitia mikutano wa hadhara Kata ya Ipinda Wilayani Kyela baada ya wananchi kulalamikia tatizo la maji lililopo katika eneo hilo.

Makalla pia aliishauri Halmashauri kutosimamia uamuzi wa kumtaka mkandarasi kuachia mradi huo akisema kuvunja mkataba kunaweza kuisababishia Serikali hasara kubwa huku wananchi wakiendelea kuteseka kwa kukosa huduma ya maji waliyoisubiri kwa miaka mingi.

Awali Mhandisi wa maji wa Halmashauri ya wilaya ya Kyela, Amos Mtweve alisema mkandarasi huyo aliongezewa muda mara tano lakini hakukamilisha mradi huo na ndipo Halmashauri ikachukua uamuzi wa kusitisha mkataba.

Mhandisi Mtweve alisema pia uamuzi wa kusitisha mkataba ulifikiwa baada ya mkandarasi kuandikiwa barua mara kadha akiitwa lakini hakuitikia wito wala kujibu barua azizopelekewa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya IRA General Enterprises Co. Limited, Isack Usaka alikiri mradi huo kuchelewa lakini akautupia lawama upande wa Halmashauri akisema yapo mambo aliyoomba yafanyiwe marekebisho lakini hayakufanyika.

Mradi wa maji wa Kapapa-Butusyo unaotarajia kuondoa adha ya maji katika vijiji nane vilivyopo wilayani Kyela ukitokea Halmashauri ya Busokelo wilayani Rungwe,ulianza kujengwa na kampuni ya IRA Julai 2014 na ulikuwa ukamilike Januari 2015 lakini hadi sasa haujakamilika.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • RC DKT. HOMERA AKUTANA NA MABALOZI WA NCHI NNE AFRIKA

    May 26, 2025
  • "WAFUNDISHENI PIA ULAJI WA LISHE WATU MAOFISINI" - RC DKT. HOMERA

    May 26, 2025
  • FISTULA INATIBIKA, MATIBABU NI BURE, KARIBU UHUDUMIWE - DKT. HOMERA

    May 19, 2025
  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa