• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mbarali Council Instructed to Prepare Land Use Plan

Imetumwa : April 24th, 2017

Kikosi Kazi cha Kitaifa cha kuokoa Ikolojia ya Mto Ruaha kimeiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali kuandaa Mpango Kazi wa Matumizi Bora ya ardhi ili kuweka ukomo wa matumizi ya ardhi kutambua kila matumizi ya ardhi, elimu ya mazingira ya Halmashauri na jinsi halmashauri iivyojipanga kuhifadhi maji ya mito iliyopo wilayani humo.

Maagizo hayo yametolewa na Kikosi Kazi cha hicho cha Kitaifa wakati wa kukusanya Maoni ya ya Wanasiasa na Watendaji wa Halmashauri ilikupata changamoto na ufumbuzi wake kuhusu kupungua kwa maji katika Mto Ruaha.

Akitoa maagizo hayo Mwenyekiti wa Muda wa Kikosi kazi hicho Mhandisi Seth Luswema amesema kuwa Halmashauri inatakiwa kuwa na takwimu sahihi za matumizi bora ya ardhi ilikujua maeneo sahihi ya matumizi ya ardhi, kujua namna ya kuhifadhi maji na pia kutoa elimu ya mazingira na uhifadhi wa maji kwa wananchi wa Wilaya hiyo.

Akichangia maoni yake kwa wajumbe wa Kikosi Kazi Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mbarali Bwana Mathayo Mwangomo amesema kuwa shughuli za kibinadamu hasa kilimo zinachangia kupunguza mtiririko wa Maji kwenda mito hii ni baada ya Serikali kubinafsisha mashamba makubwa ya mpunga mwaka 2006 na wananchi kukosa maeneo ya kulima kilimo cha umwagiliaji.

Bwana Mwangomo amesema kuwa kutokana na uchakavu wa miundombinu na mingine kujengwa kiholela kwa mtindo wa kudaka maji kutoka kwenye mifereji ya matoleo toka kwa wawekezaji na wakulima kunasababisha maji kutorudishwa kwenye mto Mbarali na kupotelea katika mashamba ya wananchi hasa kwenye Vijiji vya Ukwavila, Iyala, Mpunga Mmoja, Imalilo Songwe na  Mwendamtitu.

Naye Katibu wa CCM Abdala Mpokwa amesema kuwa Serikali inatakiwa irejee makubaliano yake na wananchi ya kujenga mabwawa ili kuwepo na uvunaji wa maji ya mvua na pia kuiomba Serikali kufanya  matengenezo ya miundombinu ya mashamba na hasa mifereji katika Kata za Luhanga, Imalilo Songwe, Ukwavila, Itamboleo na Mwantenga.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Bwana Kivuma Hamisi Msangi amesema kuwa kuna idadi kubwa ya mifugo katika halmashauri kuliko uwezo wa Wilaya hiyo kuhudumia ambapo maji yanayotumika ni mengi zaidi kuliko rasilimali iliyopo na kuchangia kukauka kwa baadhi ya mito.

 Aidha, Bwana Msangi amesema kuwa Halmashauri ina skimu 86 za umwagiliaji lakini ni skimu 5 tu zina matoleo ya maji kurudisha mtoni  kwa sababu mifereji mingi ya matoleo haisafishwi mara kwa mara na kufanya magugu maji na uchafu kuzui maji kutiririka kuelekea mitoni.

Aidha, Kikosi kazi hicho kimekuwa na wasiwasi juu ya utekelezaji wa mradi wa Skimu ya Mwendamtitu ambao unahudumia hekta 3000 za kilimo cha mpunga kwa kupoteza maji kwa wingi kutokana na miundombinu ya skimu hiyo kutengen na kufanya wananchi kuchepusha maji kiholela.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa