• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Mhe Rais Magufuli Aweka Jiwe la Msingi Ujenzi wa Maktaba MUST

Imetumwa : May 3rd, 2019



RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuliameutaka uongozi wa Chuo cha Sayansi na Teknolojia Mbeya kutumia wakandarasi ndani wanaosoma katika chuo hicho katika ujenzi wa majengo ya mabweni na maktaba ili yakamilike kwa wakati.

Mhe. Rais Magufuli ameyasema leo katika sherehe za uwekaji jiwe la msingi ujenzi wa maktaba na kuwapongeza Viongozi wa MUST kwa lengo la kupanua udahili wa wanafunzi kutoka 4630 wa sasa hadi kufikia 15000 ifikapo  2025.

Mhe.Rais Magufuli  ameahidi kutoa shilingi bilioni 2.9 na kuwataka viongozi wa chuo kutumia wakandarasi ambao wamekuwa wakitumika kujenga majengo mbalimbali ya Serikali ikiwemo shule kongwe 15, vyuo  vya maendeleo ya wananchi 18, hospitali na majengo ya wizara Mkoani Dodoma.

Mhe. Rais Magufuli amesema Serikali itahakikisha chuo hicho kinaimarishwa ili kutimiza ndoto ya Baba wa Taifa Hayati Mwl  Julius Kambarage Nyerere aliyetaka Taifa liwe na chuo imara cha Sayansi na Teknolojia na kutokana na dhamira hiyo Serikali itatoa  shilingi 5 bilioni kwaajili ya Ujenzi wa mabweni ya wanafunzi,  na kuiagiza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kutafuta fedha za kununulia vifaa vya kufundishia na kujifunzia wanafunzi.

Aidha, Mhe Rais Magufuli  amekipongeza chuo cha MUST kwa kuanzisha mafunzo ya ufundi mchundo na usadifu  na kuwaonya wanafunzi wa chuo hicho kuelekeza jitihada zao katika masomo badala ya masuala yasiyo ya msingi ikiwemo mahusiano ya kimapenzi

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe Prof. Joyce Ndalichako amemshukuru Mhe Rais Magufuli kwa kutoa kipaumbele katika elimu na amebainisha kuwa pamoja na kujengwa maktaba hiyo Serikali imetoa sh. Milioni 482.6 kwa ajili ya Ujenzi wa vyumba vya madarasa vya chuo hicho, imetoa sh milioni 702 kwa ajili ya kukarabati majengo ya chuo cha MUST kampasi ya Rukwa na sh. Milioni 483 kwa ajili ya kujenga mabweni ya wanafunzi 600 katika kampasi ya Rukwa.

Prof. Ndalichako ameongeza kuwa katika jitihada za kuboresha miundombinu ya vyuo vya elimu ya Juu Serikali imetoa shilingi bilioni 10.2 kwa ajili ya kujenga mabweni ya Chuo Kikuu cha Mzumbe  Mkoani Morogoro, ametoa shilingi bilioni 3 kwa ajili ya kujenga jengo la Taaluma na Utawala na shilingi milioni 488.3 kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya kampasi ya Tegeta  Dar-es-Salaam.                       Akisoma taarifa ya Chuo hicho Makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof. Aloys Mvuma maktaba hiyo ina ghorofa 3 na uwezo wa kuchukua wasomaji 2500 kwa mara moja ikilinganishwa maktaba iliyopo hivi sasa ambayo inachukua wasomaji 150 

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa