• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

RC Awapongeza Wananchi Kijiji Cha Ifupa

Imetumwa : July 3rd, 2020

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mh. Albert amewapongeza wananchi wa kijiji cha Ifupa Wialaya ya Mbeya kwa kuweka utaratibu wa kuwa na harambee kila siku ya Ijumaa kuchangia shughuli za maendeleo. 

Mhe Chalamila ameyasema hayo leo alipokuwa akizindua  kituo kipya cha afya Ifupa kilichopo kata ya Irungu wilaya ya mbeya vijijini ambavyo kitasaidia kutoa huduma za afya kwa wananchi wa kijiji hicho pamoja na vijiji vya jirani ambapo kata ya Irungu inavijiji saba. 

 Chalamila amewapongeza viongozi wa kijiji hicho kwa kuweza kusimamia fedha hizo vizuri na kufanikiwa kukamilisha ujenzi wa kituo hicho cha afya ambacho kitasaidia kutoa huduma mbalimbali katika kijiji hicho  

Mukugenzi wa Halmashauri hiyo Ndugu Katemba amesema Halmashauri ya wilaya ilitoa eneo lake ili liweze kutumika katika ujenzi wa kituo hicho kipya cha Afya Ifupa ambapo wananchi wa kijiji hicho pia walichangia michango yao kufanikisha ujenzi huo ambao ulianza tarehe 23/1/2017 lengo ikiwa ni kusaidia wakinamama wajawazito ambao hupata tabu pinda wakitaka kujifungua kutokana na ukosefu wa huduma za afya karibu.

Katemba ameendelea kuwa wadau mbalimbali wamechangia ujenzi wa kituo hicho cha afya ambapo TANAPA wao walichangia katika ujenzi wa nyumba ya mganga mkuu huku mbunge wa jimbo hilo alitoa mifuko 200 ya saruji 

Nae Mbunge wa Mbeya Vijijini Oren Njeza amemshukuru   Mkuu wa Mkoa wa kwa kufungua kituo chao cha Afya ili kiweze kuanza kutoa huduma na kumuomba kwa niaba ya wananchi awafikishie salamu zao kwa Mh.Rais Dr. John Pombe Magufuli kwa mchango wake mkubwa aliotoa ili kuweza kufanikisha ujenzi huo wa kituo cha afya Ifupa.


Kituo hicho kinawatumishi 6 wa afya ambapo 1 amepelekwa Muhimbili masomoni ili kuongeza ujuzi na kuja kuwapa huduma wananchi mbalimbali katika kituo hicho cha afya. 

Aidha, Mkuu wa Mkoa amewataka wananchi wa kijiji hicho kuacha migogoro ili kuendeleza maendeleo ya kijiji hicho huku akiahidi kumaliza migogoro mbalimbali inayo wakabili.

Wananchi wa kijiji cha Ifupa walimshukuru mkuu wa mkoa kwa kufika katika kijiji chao na kuweza kuendesha harambee ambayo kiasi cha fedha walichopata kitaweza kusaidia kukamilisha huduma mbalimbali katika kituo hicho huku mkuu wa mkoa akiwaahidi kurudi tena katika kijiji hicho kuona maendeleo  mbalimbali.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa