• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

RC Mbeya Atimiza Ahadi ya Saruji

Imetumwa : January 15th, 2018

MKUU wa Mkoa wa Mbeya,Amos Makalla ametimiza ahadi yake ya kukabidhi msaada wa Mifuko 100 ya Saruji kwaajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya msingi Iyela iliyopo katika kata ya Iyela jijini hapo.

Kadhalika Makalla amekabidhi msaada wa fedha taslimu shilingi milioni moja kwaajili ya kuchangia ujenzi wa vyoo katika shule ya msingi Ivumwe iliyopo katika kata ya Mwakibete jijini Mbeya.

Akikabidhi msaada huo,mkuu huyo wa mkoa alisisitiza kuwa atazidi kuwaunga mkono wananchi watakaoonesha nia ya kuibua na kuanzisha mradi wa kimaendeleo na si wale wanaobaki kusubiri kila kitu kifanywe na Serikali.

Makalla alisema wakati uliopo ni wa kila mmoja kujiuliza anawezaje kuikwamua jamii inayomzunguka kwa kubuni mradi utakaowezesha kuondokana na changamoto zilizopo kisha kuwashirikisha wadau ikiwemo Serikali.

“Yapo maeneo kila ukienda wanaorodhesha changamoto zinazowakabili,ukiwauliza ninyi mmeanza na lipi katika kutafuta ufumbuzi wanakujibu tunaisubiri Serikali ifanye.Tuna vijiji vingi,kata nyingi hapa mkoani tukisema kila hao wasubiri Serikali ikatatue changamoto tutachelewa lakini wale watakaoanzisha lazima tuwaunge mkono maana maendeleo ni ubia”alisema Makalla.

Mkuu huyo wa mkoa pia aliwasihi wakazi wa maeneo hayo kuachana na wanasiasa uchwara wanaowapotosha wananchi kuwa wadau wanaojitoa kuchangia shughuli za kimaendeleo kwa kutoa misaada wana nia ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

Alisema anachoamini yeye wadau wanaochangia maendeleo wana nia ya dhati ya kuiwezesha jamii kuondokana na changamoto zinazoikabili jamii mkoani hapa na si uchu wa madaraka.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa mtaa wa Iyela I,Simon Mwakaje alisema ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya msingi Iyela umekuwa wa kusuasua kutokana na wakazi wa eneo hilo kuwa wagumu katika kuchangia licha ya uwepo wa wadau wachache walioonesha nia ya kusaidia.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa