• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Serikali Imetoa Bilioni 9.2 Kwaajili ya Ujenzi wa Wodi ya Wazazi

Imetumwa : July 21st, 2021

Serikali ya awamu ya sita imetoa fedha zote zilizobakia na kufanya jumla ya Bilioni 9.2 kukamilisha Ujenzi wa jengo la ghorofa sita kwa ajili ya mama na mtoto katika Hospitali ya Wazazi META, mkoani hapa.

Jengo Hilo ambalo limekamilika kwa asilimia 85, linatarajiwa kuanza kutoa huduma kabla ya kumalizika mwezi Oktoba mwaka huu.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Dorothy Gwajima amefanya ziara ya dharura kukagua maendeleo ya ujenzi wa miradi mbalimbali ya afya inayoendelea mkoani humo.

Akizungumza, Waziri Gwajima amesema amefurahi kuona maendeleo mazuri ya ujenzi huo wa jengo hilo, litakapokamilika litasaidia kuimarisha huduma ya afya ya mama na mtoto.

“Mh. Rais Samia Suluhu Hassan ameshamalizia kutoa fedha zote na kufanya jumla ya Sh. bilioni 9.2 za ujenzi huu hii ni kwa kuwa anajali katika vipaumbele vinavyopunguza Kero kwenye huduma za afya hususan kero za huduma wazazi na watoto wachanga wakati wa kujifungua.

“mradi huu utakapokamilika idadi ya vitanda itaongezeka kutoka 150 hadi 400, ni jengo kubwa lenye ghorofa kama sita, limejengwa maridadi sana, lina vyumba vya kutosha na vitanda vya kujifungulia vya kutosha na vyumba vya upasuaji,” amesema.

Dkt. Gwajima ameongeza “Tumesema wajitahidi wafanye kazi usiku na mchana (kumalizia ujenzi) kufikia mwezi wa 10 wawe wamemaliza kufanya hii kazi.

Wakati huo huo, Waziri Gwajima amekagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa wodi kwa ajili ya watu wanaohitaji kufanyiwa upasuaji linalojengwa pamoja na vyumba sita vya upasuaji katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya.

“Jengo litakuwa na vitanda 82 vitakavyolaza watu waliofanyiwa upasuaji au wanaosubiri kufanyiwa upasuaji na hii ni hatua kubwa sana kuwa na vyumba vya upasuaji sita.

“Hii ni hatua kubwa sana ambayo mpaka sasa mmeshapewa hizo bilioni 3 na mnapiga hesabu kuweza kumalizia hiyo kazi iliyobaki,” amesema.

Ameagiza viongozi wa Mkoa huo kujitahidi kulimaliza mapema lisivuke mwaka huu mwezi wa nane liwe limeanza kutoa huduma.

“Mmekadiria Bilioni 5.5, fanyeni haraka hizo hesabu zije ili muweze kupewa hizo fedha hatutaki kumaliza mwaka huu hamjaanza kufanya kazi ya upasuaji kwenye haya majengo.

“Muwapunguzie pia mzigo Hospitali ya Rufaa ya Kanda kwa kuwahudumia wagonjwa wengi ambao mngeweza kuwaona ninyi pasipo ulazima wa rufaa.

“Nimefarijika kuona pia jengo la masuala yote yanayohusika na huduma za dharura kwa ufadhili wa Global Fund , limekamilika.

Ameongeza “Nimeona pia mitambo ya oksijeni iliyounganishwa na mtambo wa kufua oksijeni ambayo imesimikwa kwenye hospitali saba za mikoa na bado tunasubiri hospitali nyingine 12.

“Huu ni ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na wadau wake wakiwamo World Bank na Global Fund.

“Ndiyo maana tunasema nchi yetu inaendeshwa kwa ushirikiano na wadau mbalimbali wanaoitakia mema Serikali hii na Mh. Samia anaendelea kuweka mazingira mazuri ili tupate wadau wengi wanaoweza kushirkiana na sisi.

“Kwa kazi nzuri mliyoifanya kwa ‘force account’ hata wakija wakiangalia watafurahi, wataleta zaidi ushirikiano wa misaada mbalimbali katika kuboresha huduma za sekta ya afya,” amepongeza.

Amewataka kuhakikisha wanalikamilisha mapema ili lianze kutoa huduma na uzinduzi wa huduma ufanyike kabla ya Septemba.

“Nawapongeza mkoa na watumishi ambao mmekubali kuvumilia changamoto mbalimbali za stahiki zenu ili mpanue huduma, wateja wengi waje kisha muweze kunufaika na bima ya afya wanayotumia wengi kwa kuvutiwa na ubora wa huduma".

“Bima ya afya sheria inakuja, Mungu akisaidia kuanzia mwakani hakutakuwa na mteja anayekuja wa msamaha, kazi iliyobaki kwenu ni huduma nzuri kwa wateja na tabasamu, maana mtu mwenye hela yake anaweza kuamua kwenda zake asitumie huduma yako iwapo haimridhishi hivyo utabaki huna wateja huku miundombinu unayo.

“Haya maslahi yetu tunayosema tunachelewa kulipwa tayari Serikali imetuwekea mtaji wa miundombinu, vifaa na utaalamu tushindane kwa ubora wa huduma ‘marketing’ ili tupate wateja wengi waliojiunga na bima za afya ili hatimaye kusiwe na kuelemewa na misamaha kwa kuwa wote watakuwa na bima za afya.

“Wakija wengi kwa sababu wanapata huduma hapa, nanyi mtapata mapato mengi ya hospitali yatokanayo na mfuko wa bima, na mkumbukrle kuwa mna kamati zenu, bodi zenu hivi atakayekuja kuwapangia ni nani, tabasamu lako hela yako, anzeni hizo sera.

“Hatuombei watu waumwe lakini tumeumbiwa magonjwa hata huko ulaya walikoendelea watu wanaumwa na wanajiunga na bima hasa mtu akishakuwa kwenye bima ndugu zangu tayari huo ni uwekezaji maana ile bima ni ya afya na watakuja kupata huduma na hela hiyo itaendeleza afya kwa ujumla wake.

“ Na wakifurahia zaidi watazidi kujiunga zaidi na ninyi mtafurahi kwa kutoa huduma yenu na kuwafanya watu bima zao zitumike kwenu, tunahesabu kama miezi mingine 18 hizi kelele zingine za extra duty, on call, dawa zitakuwa hazipo, zitakuwa zimepotea.

“Msipojifunza kuyapokea haya na kujituma kwa uadilifu tutajikuta tumeachwa tupo watumishi wengi, vifaa tunavyo lakini wateja hatuna wameenda kwenye huduma bora zaidi za wenye kutabasamu.

“Kwa sababu wawekezaji watatoka nje ya nchi na matabasamu yao watakuja kuwekeza huku huku mbeya kwenye huduma hiyo hiyo unayoitoa utajikuta wewe unaulizwa na Serikali nakulipa mshahara kwa kulinda majengo, mitambo na vifaa au kwa kutoa huduma, hilo ni swali ambalo litageuka kuwa la kwetu hivyo tutafute majibu lakini tukikaa mkao wa kusubiri bima ya afya kwa wote ije, tabasamu tunalo vifaa tunavyo tutafurahi,

“Watu wataelewa na magonjwa yatatoweka yatabaki ya kinga tu, tutachukua utaalamu wenu tuendelee na kinga zaidi ,” amesema Waziri Gwajima.

Awali, akizungumza, Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Dkt.Chuwa Chuwa amemuhakikishia Waziri Gwajima kwamba watahakikisha wanasimamia maelekezo aliyoyatoa.

“Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa sisi kama Wilaya tunakushukuru sana kuja kufanya ziara katika Mkoa wetu, Watanzania wanakuona na tunafahamu namna ambavyo unahangaika kupigania afya za Watanzania tunakushukuru sana.

“kwa namna ya kipekee mwenyewe umeona na kukagua miradi ambayo ina karibu Sh. bilioni 14 ukijumlisha. Kwa kweli ni miradi mikubwa tunaomba upeleke salamu kwa Mh. Rais kazi yake aliyoifanya kwa mkoa wa Mbeya ni kubwa sana na wanambeya kiujumla wanaona namna ambavyo anahangaikia afya zao.

“Na sisi tukuahidi Mh. Waziri kwamba tutaendelea mara kwa mara hii miradi na tutaendelea kuisimamia kadri unavyotoa maelezo, hii ni mara yangu ya pili katika kipindi kifupi nilichokaa hapa, kutembelea kwenye hii miradi na mradi ambao tuliukagua kabla ya kufika hapa.

Amesema alishatoa maelekezo kwamba wafanye kazi usiku na mchana, nimemuona leo msimamizi kutoka TBA na ameniambia ameongeza muda wa kufanya kazi, muda si mrefu naamini watanzania wataanza kupata huduma kwenye miradi hii.

MWISHO

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • RC DKT. HOMERA AKUTANA NA MABALOZI WA NCHI NNE AFRIKA

    May 26, 2025
  • "WAFUNDISHENI PIA ULAJI WA LISHE WATU MAOFISINI" - RC DKT. HOMERA

    May 26, 2025
  • FISTULA INATIBIKA, MATIBABU NI BURE, KARIBU UHUDUMIWE - DKT. HOMERA

    May 19, 2025
  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa