• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Watumishi watakiwa Kuelewa Misingi ya Utumishi wa Umma

Imetumwa : September 10th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe Albert Chalamila amewataka watumishi wa umma  halmashuri ya Kyela kuelewa misingi ya utumishi wa umma na kuacha  mihemko ya kisiasa na kushindwa kuwahudumia wananchi.

Mhe.Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo leo alipokuwa akiongea na watumishi mbalimbali wa halmashauri na taasisi za umma kwenye ziara ya kujitambulisha na kusema kuwa hakuna demokrasia isiyo dhibitiwa na sheria na kanuni

Mhe Chalamila amewataka watumishi wa umma kuwa waadilifu na kutumia vizuri mamlaka waliopewa na kutokuwa chanzo cha kuongeza malalamiko ya wananchi kwa Serikali bali wametakiwa kutoa huduma bora kwa kuangalia sera na agenda ya nchi kwa sasa.

Amewataka Maafisa mipango na biashara kujitafakari wanaisaidia vipi halmashauri yao na kuagiza wataalamu hao kuwa wabunifu kwa kuandika maandiko ya kutengeneza vitega uchumi vinavyoweza kusaidia na kuiongezea halmashauri mapato ya ndani katika sekta za afya, elimu, viwanda na utalii.

Katibu Tawala wa Mkoa Bibi Mariam Mtunguja amewataka watumishi wa umma kufanya kazi kwa ushirikiano na kusema kuwa wataalamu wa kiutendaji ndio wasaidizi wakuu wa Mkuu wa Mkoa katika kutekeleza majukumu ya maendeleo katika mkoa na hivyo ni muhimu kuwa na ushirikiano wa karibu katika utendaji kazi.

Aidha, Mhe Mkuu wa Mkoa amepata fursa ya kutembelea kituo cha forodha katika Mamlaka ya Mji Mdogo Kasumulu na kukitaka kituo hicho kuongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato na kusema jambo hili linawezekana kama taasisi zote zitafanya kazi kwa pamoja ili kubadilishana ujuzi katika maeneo yao.

Ameitaka mamlaka ya forodha kukaribisha mawazo tofauti ya jinsi ya kutanua uwezo wa ukusanyaji wa mapato kwa kushirikisha mawazo mapya kutoka kwenye mamlaka nyingine ikiwa pamoja na wananchi wa eneo husika.

Mhe Chalamila ameitaka mamlaka hiyo pia kusimamia ulinzi na usalama wa mpaka kwa kuimarisha ulinzi na watu wajue kuwa mpaka unalindwa  kwani eneo hilo ni rahisi kupitika kwa wahamiaji haramu na magengo.

“kuna baadhi ya watumishi sio waadilifu katika kusimamia ulinzi wa mipaka lakini na walio waadilifu wanaitwa “wanoko”. Ni bora kuitwa “mnoko” kwa kusimamia sheria na kanuni za nchi kuliko kupendwa kwa kuvunja sheria na taratibu za Serikali” alifafanua Mkuu wa Mkoa.

Kamanda wa Polisi Mkoa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi Ulrich Matei  amewataka watumishi wa mamlaka hiyo kufanya kazi kwa kushirikiana kwa sababu mpaka huo umekuwa ukitumika sana kwa njia za panya kupitishia magendo, dawa za kulevya pamoja na wahamiaji haramu.

Kamishna Msaidizi Mwandamizi Matei amewataka pia kuangalia ulinzi na usalama wa bidhaa zinazotoka na kuingia katika mpaka huo ili kujua madhara yake na kuhakikisha wanafunga njia zote za panya zinazotumiwa na wafanyabiashara kupitisha magendo hayo.  

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa