Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Dkt. Juma Zuberi Homera hii leo amekutana na Mabalozi wa Tanzania wanaofanya Kazi Nchi Nne Afrika na kujadiliana fursa Mbalimbali za uwekezaji Kati ya Tanzania(Mkoa wa Mbeya) na Nchi hizo ikiwemo uimarishwaji wa Miundombinu ya Barabara,Reli ya TAZARA Bomba la Mafuta na Bandari Kavu ili kurahisisha Shughuli za kibiashara.
Mabalozi waliofika Ofsini ni Pamoja na Balozi wa Tanzania Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo(DRC) Said Mshana, Agness Kayola Balozi Nchini Malawi, Mathew Mkingule Balozi nchini Zambia, Magabilo Murobi Balozi Mdogo Lubumbashi na Afisa Biashara Kutoka Zambia John Ngowo ambao wamefika Kuhudhuria Maongesho ya Kibiashara ya Mbeya Expo 2025.
Aidha RC Dkt. Homera amesema Eneo la Tanganyika Packers na eneo la TBC ni Moja ya Maeneo ambayo Mbeya imeyatenga Maalumu kwaajiri ya uwekezaji wa Viwanda na Shughuli zingine, ambapo Nchi Jirani na Tanzania zinaalikwa Kuna kufanya uwekezaji huo.
Matarajio Mema ya kuwa na Mji wa Kisasa Kata ya Nsalala Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Ukamilishwaji wa Barabara Njia Nne ni Moja ya vitu vinavyotazamiwa kuongeza Chachu ya uwekezaji Mbeya.
"Sisi Mbeya tuko Vizuri kwenye kilimo tunazalishaji zao la Kakao,Parachichi,Mpunga, Tumbaku, Pareto Chai na Kahawa hivyo tunawezafanya uwekezaji Mkubwa kupitia Kilimo hiki" RC Homera amesema.
Kwa Upande wao Mabalozi wameyapokea Maombi ya Dkt . Homera na kuahidi kuyachukua na kuzungumza na Wawekezaji wa Nchi wanazofanyia Kazi kwa kusudio la kuongeza mashitikiano Mema.
2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA
Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.
Simu: 025-2504045
Simu ya Mkononi:
Barua pepe: ras@mbeya.go.tz
Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa