Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Dkt. Juma Z. Homera amewataka Maafisa Lishe wa Halmashauri kufundisha Umhimu wa Lishe kwa Watu wazima ili kuzingatia Namna bora ya ulaji badala ya kula Vyakula vya aina Moja vinavyoweza kuchangia Hali ya Ukondefu na udumavu kwa Watoto.
Homera ameyasema hayo hii leo akiwa kata ya Inyala Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya wakati akizindua Mradi wa Lishe ya Mwanao unaotekelezwa na Shirika la CRS chini ya udhamini wa Serikali ya Norway kwa Kushirikiana na UNICEF.
Katika Uzinduzi wa Mradi huo unaotekelezwa katika Mikoa ya Mbeya na Njombe Dkt.Homera amesema kiwango Cha ukondefu kimepungua Kutoka asilimia 2.7 hadi asilimia 0.6, Uzito pungufu(Udumavu) umepungua Kutoka asilimia 9.8 mpaka asilimia 1.4 wakati Uzito uliozidi umepungua Kutoka asilimia 5.3 hadi asilimia 5.2
Akisoma Taarifa ya Mradi Bi Ophilia Katumuna Kutoka UNICEF amesema Lengo la Mradi ni Kupunguza udumavu wa utotoni na kuboresha Matokeo ya Lishe ya Vijana kwa kupitia miundo na mifumo ya Jamii iliyoimarishwa kwa kuwa Udumavu huathiri ukuaji wa kimwili na wa kiakili kwa Watoto.
Ophilia amesema Hali ya Udumavu kwa Mkoa wa Mbeya ni asilimia 32 ambao ni juu kidogo ya wastani wa kitaifa ambao ni asilimia 30 ikizingatiwa kuwa Mkoa wa Mbeya ni miongoni mwa Mikoa inayozalidha mazao ya Chakula kwa wingi kwa Kipindi chote Cha Mwaka.
Kwa Upande Wake Dorice Munisi Meneja Mradi wa Lishe ya mwanao Mkoa wa Mbeya Kutoka CRS Walengwa wa Mradi ambao Watoto chini ya Miaka mitano na Wazazi wao, Mama wajawazito,Vijana wa Rika balehe, wanaume vinara Pamoja na Jamii kwa Ujumla
Afua mahususi za Lishe na afua mtambuka za Lishe miongoni mwa afua mahususi za Lishe ni kukuza na kuhamasisha ulishaji wa watoto wachanga na wadogo, kukuza na kuongeza matumizi ya Vyakula vilivyoongezwa virutubishi, kuimarisha ufuatiliaji na ukuaji wa Mtoto na uhamasishaji na kuboresha Hali ya Lishe mashuleni.
2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA
Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.
Simu: 025-2504045
Simu ya Mkononi:
Barua pepe: ras@mbeya.go.tz
Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa