• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mbeya Region
Mbeya Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mbeya

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mipango na Uratibu
      • Elimu
        • Orodha Mpya ya Vitu
      • Uwekezaji, Viwanda na Biashara
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Tehama na Takwimu
      • Fedha
      • Manunuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Mbeya
    • Chunya
    • Mbarali
    • Rungwe
    • Kyela
  • Halmashauri
    • Kyela
    • Busokelo
    • Mbeya
    • Chunya
    • Rungwe
    • Mbarali
    • Jiji la Mbeya
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Ziwa Ngozi
      • Milima ya Mbeya
      • Daraja la Mungu
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Kilimo
    • Maji
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Nyaraka
    • Sheria
    • Fomu ya Maombi
    • Mpango Mkakati
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi/Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha

Serikali Yatoa zaidi ya Shillingi Bilioni 3 kwaajili ya Ujenzi wa Barabara

Imetumwa : March 1st, 2018

SHILINGI Bilioni 3.7 zimetolewa na Serikali kwa ajili ya kuboresha miradi ya ujenzi barabara mbalimbali itakayotekelezwa Jijini Mbeya kwa kiwango cha lami na kusimamiwa na Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA)

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe Amos Makalla alibainisha hayo kwenye uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa kipande cha barabara cha kutoka Isyesye hadi Relini jijini Mbeya chenye urefu wa kilomita 2.3.

Mhe Makalla amesema ujenzi wa kipande hicho cha barabara kitakachonufaisha kata za Isyesye na Itezi utagharimu Shilingi milioni 881.

Amesema kuwa Serikali imetenga fedha hizo kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami jijini hapa na kurahisisha shughuli za usafirishaji kupitia miundombinu rafiki.

Aliwapongeza wakazi wa kata ya Isyesye waishio jirani na barabara kwa ushirikiano walioonesha kwa Serikali kwa kukubali kwa hiyari kubomoa bila fidia sehemu ya nyumba zilizokuwa ndani ya eneo linalopaswa kufikiwa na barabara.

 “Serikali inapenda watu walio na ushirikiano. Na ndiyo sababu sisi tumejipanga popote walipo wananchi wanaoonyesha ushirikiano tutapeleka miradi. Hatutaki watu wanaokaa kuhamasisha itikadi za vyama badala ya Kuhamasisha maendeleo katika maeneo yao” alisisitza Makalla.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Isyesye, Bw Ibrahim Mwampwani alisema barabara ya lami ilikuwa ikisubiriwa kwa muda mrefu na wakazi wa kata za Isyesye na Itezi kutokana na adha waliyokuwa wakiipata hususani nyakati za mvua nyingi.

Alisema kujengwa kwa barabara hiyo kutakuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo situ kwa wakazi wa kata hizo mbili bali na maeneo mengine kwakuwa watu wengi wataitumia badala ya kulazimika kupita barabara kuu pekee.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UTAMILIFU "MOCK" KIDATO CHA NNE MKOA WA MBEYA 2024 August 20, 2024
  • FOMU YA MAOMBI YA USHIRIKI WA MAONESHO YA NANENANE 2024 July 23, 2024
  • Fomu ya Maombi Ushiriki wa Maonesho ya Nanenane_2023-_Kiswahili July 03, 2023
  • WANAFUNZI WALIOPANGWA KATIKA VITUO VYA UFUNDI STADI NA ELIMU NJE YA MFUMO RASMI MKOA WA MBEYA February 03, 2023
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • MAANDALIZI YA SHEREHE ZA NANE NANE NYANDA ZA JUU KUSINI YAANZA KWA KISHINDO

    April 30, 2025
  • MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WAHIMIZWA KUTUMIA MFUMO WA IMES

    April 29, 2025
  • TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI YARIDHISHWA NA MAJIBU YA WADAU KUHUSU MAPENDEKEZO UGAWAJI WA JIMBO LA MBEYA MJINI.

    April 25, 2025
  • DKT. HOMERA AAGIZA MRADI KUKAMILIKA HARAKA IWEZEKANAVYO ILI WANANCHI WAPATE HUDUMA

    April 14, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

MAONESHO YA NANENANE KITAIFA MBEYA
Video

Viunganishi vya Haraka

  • Mbeya Regional GNP Report 2015
  • Barua Pepe za Watumishi
  • Mbeya kwa Namba
  • Utaratibu wa Uhamisho
  • Fomu ya Ruhusa
  • Maoni na Malalamiko
  • Mafanikio ya TASAF
  • OPRAS Fomu
  • Fomu ya Matibabu

Viunganishi Linganifu

  • Sekretarieti ya Ajira
  • EOFFICE
  • Utumishi
  • Ikulu
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiria Nje ya Nchi
  • Tovuti ya Serikali

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    2 Barabara ya Kamishina, 53180 MBEYA

    Anuani ya Posta: P. O.Box 754,Mbeya.

    Simu: 025-2504045

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras@mbeya.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Haki Miliki©2023 Mkoa wa Mbeya. Haki zote Zimehifadhiwa